// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MAJANGA ARSENAL, KOSCIENLY, SZCZESNY NA GIROUD WAUMIA MAZOEZINI NAGOYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MAJANGA ARSENAL, KOSCIENLY, SZCZESNY NA GIROUD WAUMIA MAZOEZINI NAGOYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Sunday, July 21, 2013

        MAJANGA ARSENAL, KOSCIENLY, SZCZESNY NA GIROUD WAUMIA MAZOEZINI NAGOYA

        IMEWEKWA JULAI 21, 2013 SAA 2:37 USIKU
        KOCHA Arsene Wenger amepata pigo tena katika safu yake ya ulinzi leo, baada ya Laurent Koscielny kugongana na kipa Wojciech Szczesny mazoezini na kuumia, hivyo ataukosa mchezo wa kirafiki kesho mjini Nagoya.
        Beki Mfaransa, Koscielny alitoka kwenye mazoezi mwishoni akionekana kama aliyeumia kifundo cha mguu wa kulia.
        Mara moja alitazamwa na dawati la tiba la The Gunners juu ya maumivu yake, kabla ya kupelekwa Uwanja wa Rugby wa Mizuno kwa uchunguzi zaidi.
        Larking about: Laurent Koscielny was in high spirits in Sunday's training session before picking up a knock
        Laurent Koscielny alikuwa na morali ya hali ya juu katika mazoezi ya leo kabla ya kuumia
        Popular: Theo Walcott signs autographs for the baying fans in Nagoya
        Theo Walcott akisaini autographs kwa mashabiki Nagoya
        Arsene Wenger
        Arsene Wenger
        Arsene Wenger akizungumza na mashabiki wakati wa mazoezi

        Ukubwa wa maumivu yaked bado haujajulikana, lakini anaonekana hatacheza mechi ya kesho.
        Benchi la Ufundi la Arsenal litafuatilia tatizo kwa saa 24, lakini wanaamini halitakuwa tatizo la muda mrefu.
        Na katika pigo lingine, Szczesny naye anaweza kuukosa mchezo wa kesho kutokana na maumivu.
        Crowd control: Security guards hold back the fans as they await the stars' arrival
        Walinzi wakiwadhibiti mashabiki waliokuwa wanasubiri nyota wa Arsenal wawasili
        Sign here: Bacary Sagna makes his way through the crowd before Arsenal's training session
        Saini hapa: Bacary Sagna akipasua katika ya umri ya mashabiki wakati Arsenal inakwenda kufanya mazoezi
        Warming up: The Arsenal squad warm up before a training session in Japan
        Kikosi cha TArsenal kikipasha nchini Japan
        Happy to be here: England duo Alex Oxlade-Chamberlain and Theo Walcott pose for a photo during training
        Furaha kuwa hapa: Wachezaji wa England, Alex Oxlade-Chamberlain na Theo Walcott wakipozi kwa picha wakati wa mazoezi

        Mpland huyo inafahamika aliumia mazoezini tangu wawasili Japan Ijumaa asubuhi.
        Aisha, Lukasz Fabianski au Damien Martinez mmojawapo atachukua nafasi ya Szczesny dhidi ya Nagoya Grampus.
        Habari za kuumia kwa Koscielny zinamaanisha Wenger ambaye kwa sasa tayari anamkosa beki wake mmoja mzoefu, Per Mertesacker katika ziara hii ya Mashariki ya Mbali; atamtumia kinda Ignasi Miquel kikosini.
        Wenger tayari anamkosa Thomas Vermaelen, ambaye yuko nje kwa miezi mitatu kwa majeruhi.
        Popular figure: Walcott has a fair few autographs to get through before he can get into training
        Walcott akisaini autographs kabla ya kuingia mazoezini
        All smiles: Lukas Podolski poses for the cameras from the team bus
        Lukas Podolski akipozi kwa ajili ya kamera akiwa ndani ya basi la timu
        Happy snapper: Podolski turns photographer during a training session in Japan
        Mpiga picha: Podolski aligeuka mpiga picha wakati wa mazoezi Japan
        Watching on: Per Mertesacker during a training session in Japan
        Per Mertesacker mazoezini Japan

        Maumivu ya Koscielny yanaweza kumfanya Wenger aharakishe jitihada za kumsajili sentahafu wa Swansea, Ashley Williams anayemuwania kwa muda mrefu.
        Mshambuliaji Olivier Giroud, ambaye ni mfungaji bora wa klabu katika mechi hizi za kujiandaa na msimu, akifunga mabao matano katika mechi mbili, pia aliumia mazoezini, lakini akainuka na kuendelea.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: MAJANGA ARSENAL, KOSCIENLY, SZCZESNY NA GIROUD WAUMIA MAZOEZINI NAGOYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry