Saturday, June 08, 2013

    BALOTELLI APIGA NGUMI UKUTA BAADA YA KULIMWA NYEKUNDU

    IMEWEKWA JUNI 8, 2013 SAA 6:38 MCHANA
    MSHAMBULIAJI Mario Balotelli alipiga ngumi ukuta baada ya kulimwa kadi nyekundu Italia ikitoka sare ya 0-0 na Jamhuri ya Czech mjini Prague.
    Mshambuliaji huyo wa AC Milan alitolewa nje zikiwa zimesalia dakika 20 lakini akawawakia refe na benchi la ufundi la Italia na viongozi, kabla ya kumalizia hasira zake kwa kupiga ngumi ukuta wakati anatoka nje.
    VIDEO Mario Balotelli akilimwa kadi nyekundu Prague
    Anger: Mario Balotelli vents his frustrations on a wall after being sent off against the Czech Republic
    Hasira: Mario Balotelli akimalizia hasira zake kwa kupiga ngumi ukutani


    And he's off: Mario Balotelli is sent off for two yellow cards against the Czech Republic
    Nenda nje: Mario Balotelli akionyeshwa kadi nyekundu
    Unfair: Balotelli doesn't think he should've been sent off for the challenge on Theodor Gebre Selassie
    Si haki: Balotelli hakuona kama alistahili kupewa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Theodor Gebre Selassie
    Play acting: Balotelli thought Gabre Selassie made the most of the contact
    Balotelli anaondoka huku Gabre Selassie akilalamika chini

    Faulo iliyomponza alimchezea beki wa kulia wa Czech, Theodore Gabre Selassie, baada ya Balotelli kumpa mkono wa usoni beki huyo wakati wa kugombea mpira.
    Sare hiyo inaiweka kileleni mwa Kundi B Italia katika mbio za kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia, kwa pointi nne zaidi ya Bulgaria walio nafasi ya pili. 
    Czech inabaki nafasi ya tatu, nyuma ya Bulgaria.

    Group B

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BALOTELLI APIGA NGUMI UKUTA BAADA YA KULIMWA NYEKUNDU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry