• HABARI MPYA

        Sunday, March 17, 2013

        ZOLA WA YANGA KUZIKWA KESHO KISUTU, MSIBA UPO JANGWANI

        Hamza Said 'Zola' enzi
        za uhai wake

        Na Mwandishi Wetu
        ALIYEKUWA mhudumu wa klabu ya Yanga SC, Hamza Said maarufu kama Zola au Chiluba aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari, anatarajiwa kuzikwa kesho Saa 10:00 jioni katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.
        Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kwamba kifo cha Hamza ni pigo kwa klabu, kwani alikuwa mchapakazi, mwaminifu na aliyejitolea mno kwa ajili ya klabu yake aipendayo.
        Alisema msiba upo makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani Dar es Salaam na ameomba wapenzi na wanachama kujitokeza kwa wingi kesho kumsindikiza mwenzao katika safari yake mwisho.
        Hamza alikutwa na umauti alfajiri ya leo, baada ya kugongwa na gari katika makutano ya Mitaa ya Rufiji na Kongo. Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: ZOLA WA YANGA KUZIKWA KESHO KISUTU, MSIBA UPO JANGWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry