• HABARI MPYA

        Tuesday, March 19, 2013

        MANJI AZINDUA BARAZA LA WADHAMINI YANGA, BALOZI MPUNGWE, MH MKUCHIKA NDANI

        Mwenyekiti wa Yanga SC, ALhaj Yussuf Mehboob Manji akimkabidhi Katiba ya Yanga, Mjumbe wa Baraza jipya la Wadhamini la klabu hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Mh. George Huruma Mkuchika (kushoto) jioni ya leo, makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam. 

        Manji kushoto akimkabidhi Katiba ya Yanga, Mjumbe mwingine, Balozi Ammy Mpungwe

        Manji akimkabidhi Katiba, Mjumbe mwingine, Francis Mponjoli Kifukwe kulia

        Manji kushoto akimuonyesha Mh. Mkuchika mali za klabu zilizopo makao makuu ya klabu

        Mkuchika pembeni ya Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga akishika moja ya mashine za gym za klabu hiyo

        Balozi Mpungwe akifanya mazoezi kwenye moja ya mashine za gym za klabu hiyo

        Francis Kifukwe kulia akiwaonyesha ukubwa wa eneo la Yanga maeneo ya Jangwani, Mh Mkuchika na Balozi Mpungwe

        Mh Mkuchika akiuliza zaidi kwa Kifukwe kuhusu ukubwa wa eneo la klabu

        Katibu wa Yanga, Lawrence Mwalusako kushoto akiwaonyesha Mh Mkuchika na Balozi Mpungwe vyumba vya wachezaji katika jengo hilo  

        Katika picha ya pamoja ni viongozi wa Yanga Wajumbe wa Baraza la Wadhamini
        Mwanachama wa Yanga, Thomas Mdeka akifurahia Bodi ya Wadhamini kwa kusema; Yanga oyeeeee
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: MANJI AZINDUA BARAZA LA WADHAMINI YANGA, BALOZI MPUNGWE, MH MKUCHIKA NDANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry