• HABARI MPYA

        Sunday, November 04, 2012

        KADO APATA AJALI AKIELEKEA MOROGORO KWENYE GAME LA SIMBA

        Kado

        Na Mahmoud Zubeiry
        KIPA namba moja wa Mtibwa Sugar, Shaaban Hassan Kado amepata ajali ya gari leo akiwa anaelekea Morogoro, ambako timu yake inamenyana na Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo.
        Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, Kado alikuwa anakwenda Morogoro kujiunga na wenzake kambini, akitokea nyumbani kwao Dar es Salaam.
        Alipoulizwa kwa nini kipa huyo hakuwa kambini wakati timu yake ina mechi leo, Mexime alisema; “Kado anatumikia adhabu ya kadi nyekundu, kwa hivyo hayuko kwenye programu ya mechi ya leo. Alikuwa ana ruhusa fupi ya kwenda kwao,”alisema.
        Mexime alisema Kado alipata ajali kwanza kwa gari yake anaelekea Morogoro, na akaiacha na kupanda gari kurudi Dar es Salaam na akiwa kwenye gari hilo lingine, kipa huyo wa zamani wa Yanga alipata tena ajali.
        “Baada ya ajali hiyo mimi ndio nikamfuata kwenda kumchukua na sasa niko naye njiani tunaelekea Morogoro moja kwa moja hospitali,”alisema.
        Hata hivyo, Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars alisema Kado hajaumia sana, amepata michubuko kidogo tu kichwani kutokana na kuchanwa na kioo cha gari na zaidi anasema anasikia maumivu sehemu ya kiuononi.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: KADO APATA AJALI AKIELEKEA MOROGORO KWENYE GAME LA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry