// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); WACHEZAJI TAIFA STARS WAPEWA 'NENO' NA MKUU WA MKOA DAR - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE WACHEZAJI TAIFA STARS WAPEWA 'NENO' NA MKUU WA MKOA DAR - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
    Thursday, June 14, 2012

    WACHEZAJI TAIFA STARS WAPEWA 'NENO' NA MKUU WA MKOA DAR


    Mkuuwa Mkoa wa Dar es Salaam, Meckysadik kulia akimkabidhi bendera, Nahodha wa Taifa Stars, Juma Kaseja kushoto katika hoteli ya Tansoma asubuhi ya leo. Anayemfuatia Meckysadik ni Kocha wa Stars, Kim Poulsen.  

    MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meckysadik amewataka wachezaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kuhakikisha wanadumisha viwango vyao kama wachezaji wa nchi nyingine, badala ya desturi iliyozoeleka ya wachezaji wa nchi hii ‘kufulia’ mapema kisoka.
    ‘Bosi’ huyo wa Jiji la Dar es Salaam, ameyasema hayo mchana wa leo kwenye hoteli ya Tansoma, eneo la Gerezani, Kariakoo katika hafla fupi ya kuwaaga wachezaji wa Taifa Stars na kuwakabidhi bendera kwa ajili ya mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani nchini Afrika Kusini, dhidi ya Msumbiji Jumapili mjini Maputo.
    “Nawaomba mjitahidi kudumisha viwano vyenu kama ilivyo wachezaji wa wenzetu, wanacheza mpira kuanzia wana miaka 18 na wanaendelea hadi wakifika miaka 30, sasa naomba na nyinyi iwe hivyo, siyo kama ilivyo sasa, mchezaji wa Tanzania anaibuka, baada ya mwaka mmoja au miwili anapotea,”alisema.
    Pamoja na hayo, kuelekea mchezo huo na Msumbiji Jumapili, ambao Stars inatakiwa itoke sare ya 2-2 au zaidi ili kusonga mbele, baada ya awali kulazimishwa sare ya 1-1 na Mambas mjini Dar es Salaam, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Stars wakapiganie ushindi.
    “Mimi huwa sipendi haya mambo ya kupigiana mahesabu, siyo mazuri. Kama sasa hivi kwenye Euro 2012 kuna timu zinapigiana mahesabu, kwa sababu zimelingana kila kitu. Mimi ninataka mkashinde, kapiganieni ushindi,”alisema Meckysadik.
    Mapema, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Chillah Tenga aliwaambia wachezaji wa Taifa Stars kwamba, mwanafunzi mzuri ni yule anayeendelea kujifunza kila siku kwa juhudi na si yule anayejiona tayari amejua na kubweteka.
    Kwa sababu hiyo, Tenga akawataka Stars wakacheze kwa juhudi zaidi Msumbiji na si kujiona wamefuzu baada ya kuifunga Gambia, mabao 2-1 Jumapili katika mchezo wa Kundi C, kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014.
    Kwa upande wake, kocha wa Taifa Stars, Mdenmark Kim Poulesen amesema kwamba wanaelekea kwenye mchezo mgumu, lakini watapigana kwa juhudi kupata ushindi, ili kufanikiwa kuingia kwenye hatua ya makundi katika kuwania tiketi ya Afrika Kusini 2013.
    Poulsen ambaye huo, utakuwa mchezo wake wa nne tangu aanze kazi akirithi mikoba ya Mdenmark mwenzake, Jan Poulsen baada ya awali kuiongoza timu hiyo katika sare ya 0-0 na Malawi Dar es Salaam, kichapo cha 2-0 kwa Ivory Coast mjini Abidjan na ushindi wa 2-1 na Gambia, amesema vijana wake wanaendelea kuimarika kila kukicha na ana matumaini nao makubwa.
    Anasikitika tu jana kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy Jr.’ aliumia mazoezini, ingawa amesema anaendelea na matibabu na wataenda naye Msumbiji.
    Kwa upande wake, Nahodha Juma Kaseja alisema kwamba wanatambua ugumu wa mchezo huo kwao, lakini watakwenda kupigana ‘kufa na kupona’. Kaseja amesema kwamba soka siyo tufe kwamba kila siku liko vile vile, bali inabadilika na sasa timu yao imebadilika mno na Watanzania watarajie matokeo mazuri Jumapili.
                   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WACHEZAJI TAIFA STARS WAPEWA 'NENO' NA MKUU WA MKOA DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry