• HABARI MPYA

        Saturday, June 30, 2012

        TWENDENI TUKAONE SILAHA MPYA ZA YANGA TAIFA LEO


        Na Prince Akbar
        MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Yanga SC leo wanashuka dimbani kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kumenyana na mabingwa wa Uganda, Express ‘Red Eagles’ katika mchezo wa kirafiki, wenye lengo la kuwatambulisha wachezaji wake.
        Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu ameiambia BIN ZUBEIRY maandalizi yote ya mchezo huo yamekamilika na amewataka wapenzi wa Yanga kumiminika kwa wingi uwanjani kuwaona wachezaji wao wapya.
        Sendeu amesema kwamba wachezaji wote wapya wa Yanga watapewa nafasi leo, ili kuanza kuzoeana na mashabiki wa klabu hiyo.
        Miongoni mwa wachezaji wapya wa Yanga, wanaotarajiwa kuwa kivutio leo ni kipa Ally Mustafa Mtinge ‘Barthez’, beki Kelvin Yondan wote kutoka Simba, beki Juma Abdul kutoka Mtibwa Sugar, beki Ladislasu Mbogo kutoka Toto African, viungo Nizar Khalfan aliyekuwa anacheza Marekani, Frank Damayo kutoka JKT Ruvu, washambuliaji Said Bahanuzi ‘Ortega’ kutoka Mtibwa Sugar na Ally Msuva kutoka Moro United.
        Lakini pia bado wachezaji wa zamani wa klabu hiyo, kama Hamisi Kiiza, Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo, Jerry Tegete, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wataendelea kuwa kivutio katika klabu hiyo.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: TWENDENI TUKAONE SILAHA MPYA ZA YANGA TAIFA LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry