• HABARI MPYA

        Friday, June 29, 2012

        SIMBA KUANZA NA URA, YANGA NA WARUNDI KAGAME, AZAM WAPEWA WAZENJI


        Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye kulia akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za TFF, mchana huu. Kushoto ni Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah.

        Na Prince Akbar
        MABINGWA watetezi wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame watafungua dimba na Atletico ya Burundi katika mchezo wa Kundi C wa michuano hiyo, Julai 14, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati wapinzani wao wa jadi, Simba SC waliowekwa Kundi A, wataanza na URA ya Uganda Julai 16, kwenye Uwanja huo huo.
        Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano hiyo, Azam FC wao wataanza na Mafunzo ya Zanzibar katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Chamazi, Julai 15.
        Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholaus Musonye amesema katika Mkutano na Waandishi wa Habari mchana huu, ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ilala, Dar es Salaam kwamba, Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itashiriki kama timu mualikwa.
        Aidha, habari za kusikitisha ni kwamba, Musonye amesema Sudan, Ethiopia, Eritrea na Somalia hazitaleta wawakilishi wao kwa sababu mbalimbali.
        Wakati Ethiopia ligi yao inaanza wiki hii, Sudan wawakilishi wao wapo kwenye michuano ya Afrika na wameshindwa kuteua timu mbadala, Somalia wawakilishi wao Elman wamebadilisha uongozi, hivyo bado hawajajipanga na Eritrea kutokana na desturi ya wachezaji wao kuzamia kila wanapokuja kwenye mashindano, wameondolewa.
        “Wameondolewa, kwa sababu mbili, kwanza nchi yao imeomba ipewe muda kulifanyia kazi sual hilo, na sisi pia (CECAFA) tunalitafutia ufumbuzi,”alisema Musonye.  
        Lakini Musonye amekiri kitendo cha kuyatoa mashindano hayo mwanzoni mwa mwaka hadi katikati ya mwaka kumechangia baadhi ya timu kutoshiriki na amesema tayari amewasilisha pendekezo kwenye Mkutano Mkuu, mashindano yarejee kufanyika mwanzoni mwa mwaka kama ilivyokuwa awali.
        Kuhusu mechi ya ufunguzi ya Simba kuchezwa Julai 16, ambayo itakuwa Jumatatu badala ya Jumapili, Musonye alisema kwamba imetokana na kwamba Julai 15, Uwanja wa Taifa kutakuwa na fainali za Copa Coca Cola, ambayo maandalizi yake yote yamekamilika.
        Yanga ndiye bingwa mtetezi wa mashindano, baada ya kuifunga Simba SC katika fainali mwaka jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



        CECAFA CLUB KAGAME CUP 2012
        14th – 28th July 2012, Dar-Es Salaam, Tanzania
        Team Fixture list
         
        GROUP A             SIMBA(TZ), URA (UGA), VITA CLUB (CONGO DR) PORTS (DJB),
        GROUP B             AZAM(TZ), MAFUNZO(ZANZ), TUSKER (KEN),  
        GROUP C             YANGA(TZ), APR(RWD),WAU SALAAM (SOUTH SUDAN), ATLETICO(BUR),
         
        (QUALIFICATION: GROUP A 1st and 2nd AND 3rd GROUP B 1st and 2nd , GROUP C 1st and 2nd  AND 3rd QUALIFY TO QUARTER FINALS).
         
        DATE
        NO
        TEAMS
        GROUP
        VENUE
        TIME (EAT)
        Sat 14th July
        1
        2
        APR Vs WAU SALAAM
        YANGA v ATLETICO
        C
        C
        Dar
        Dar
        2pm
        4 PM
        Sun 15THJuly
        3
         
        AZAM V MAFUNZO
         
        B
         
        CHIMANZI
        4 PM
        Mon 16th July
        4
        5
        VITA CLUB Vs PORTS
        SIMBA Vs URA
        A
        A
        Dar
        Dar
        2PM
        4PM
        Tue 17th July
        6
        7
        ATLETICO Vs APR
        WAU SALAAM Vs YANGA
        C
        C
        Dar
        Dar
        2pm
        4PM
        Wed 18th July
        8
        9
        VITA CLUB Vs URA
        PORTS  Vs SIMBA
        A
        A
        Dar
        Dar
        2 pm
        4pm
        Thu 19th July
        10
        11
        ATLETICO Vs WAU Salam
        MAFUNZO Vs TUSKER
        C
        B
        Dar
        Dar
        2pm
        4pm
        Fri 20th July
        12
        13
        PORTS Vs URA
        YANGA Vs APR
        A
        C
        Dar
        Dar
        2pm
        4pm
        Sat 21st July
         
        14
        15
         
         
        AZAM Vs TUSKER
        SIMBA Vs VITA CLUB
         
         
        B
        A
         
         
        TBD
        TBD
        TBD
        TBD
         
        TBD
        Sun 22nd July
         
        REST DAY
         
         
         
         
         
        QUARTER FINALS
        Mon 23th July
        16
        17
        B2 Vs C2
        A1 Vs C3
         
         
        TBD
        TBD
        Tue 24th July
        18
        19
        C1 Vs A2
        B1 VsA3
         
        TBD
        TBD
        Wed 25th July
         
        REST DAY
         
         
        SEMI FINALS
        Thu 26th July
        20
        Winner 16 Vs Winner 17
         
        TBD
        TBD
        Thu 26th July
        21
        Winner 18 Vs Winner 19
         
        TBD
        TBD
         Fri 27th July
        REST DAY
        FINALS AND 3rd PLACE PLAY OFFS
        Sat 28th July
        22
        23
        Loser 20 Vs Loser 21
        Winner 20 Vs Winner 21
         
         
        TBD
        TBD
         

        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: SIMBA KUANZA NA URA, YANGA NA WARUNDI KAGAME, AZAM WAPEWA WAZENJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry