// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KABURU: TUNAWASHITAKI YANGA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KABURU: TUNAWASHITAKI YANGA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Wednesday, June 06, 2012

        KABURU: TUNAWASHITAKI YANGA


        MAKAMU Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba wataishitaki Yanga kwa kitendo cha kuzungumza na beki wao, Kelvin Patrick Yondan kinyume cha kanuni za usajili.
        Akizungumza na BIN ZUBEIRY dakika chache zilizopita, Kaburu (pichani kushoto) alisema kwamba kanuni za usajili haziruhusu klabu kuzungumza na mchezaji wa klabu nyingine bila kupewa ruhusa na klabu yake.
        “Kwa mujibu wa fomu tuliyoiona ambayo Yondan amesaini Yanga, wakati anasaini Yanga alikuwa ana mkataba wa miezi sita na Simba, kisheria ni makosa na sisi tutawashitaki kwa kukiuka kanuni za usajili,”alisema.
        Inadaiwa Yondan alisaini Yanga, Novemba mwaka jana- wakati ambao wenyewe (Yanga) wanadai alikuwa hana mkataba na Simba SC.
        Yondan mwenyewe amekwishakaririwa akikana kusaini Yanga, ingawa fomu ya mkataba imemuumbua leo. Mapema mwezi uliopita Simba ilisema ilikwishongeza mkataba na Yondan.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: KABURU: TUNAWASHITAKI YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry