// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); AZAM FC KAMBINI IJUMAA SHAMBA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE AZAM FC KAMBINI IJUMAA SHAMBA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
    Wednesday, June 06, 2012

    AZAM FC KAMBINI IJUMAA SHAMBA


    Wachezaji wa Azam

    BAADA ya mapumziko ya takribani mwezi mmoja tangu kumalizika kwa msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, wachezaji wa Azam FC wameanza kuwasili mjini Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Kagame.
    Meneja wa Azam FC, Patrick Kahemele ameiambia BIN ZUBEIRY asubuhi hii kwamba,
    kulingana na programu ya maandalizi, Azam FC wataanza mazoezi Ijumaa wiki hii, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi maalum kwa mashindano hayo yatakayofanyika mwezi ujao mjini Dar es Salaam.
    Kahemele amesema wachezaji kutoka nje ya Tanzania watawasili mapema wiki hii kwa maandalizi ya makazi kabla ya kuanza kwa mazoezi hayo yatakayofanyika kwenye Uwanja wa Azam, Chamazi.
    Alisema usajili kwa wachezaji ulikwishamalizika kabla ya wachezaji kwenda likizo, hivyo wachezaji wote waliosajiliwa wataanza mazoezi isipokuwa wale walioko kwenye timu zao za taifa, Tanzania, Uganda na Zanzibar, ambazo zipo kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa wikiendi hii.
    Alisema programu ya maandalizi ya Kombe la Kagame, itamalizika siku moja kabla ya kuanza mashindano hayo na yatakapomalizika, wachezaji watapewa mapumziko ya siku chache kabla ya kuanza maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.
    Kahemele amesema maandalizi kwa ajili ya VPL yatahusisha pia ziara ya nje ya nchi ya kujiandaa na msimu mpya, ingawa amesema nchi hiyo itatajwa baadaye.
    Kahemele alisema wachezaji wapya kiikosini Azam msimu huu ni kiungo Mkenya George ‘Blackberry’ Odhiambo na kipa Deogratius Munishi kutoka Mtibwa Sugar, wakati Aishi Salum, Jackson Wandwi, Dizana, Ibrahim Rajab Jeba na Joseph Kimwaga, wamepandishwa kutoka akademi ya Azam.
    Kikosi kamili cha Azam FC kinaundwa; na makipa, Mwadini Ally, Deo Munishi ‘Dida’ Aishi Salum na Jackson Wandwi, mabeki wa Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Samir Haji Nuhu, Luckson Kakolaki, Said Mourad, Joseph Owino na Aggrey Morris.
    Viongo ni Kipre Bolou, Abdulhalim Humud, Himid Mao, Salum Abubakar, Abdi Kassim Sadalla, Ramadhani Suleiman Chombo, Abdulghani Ghullam, Ibrahim Rajab Jeba, Jabir Aziz Stima, Ibrahim Joel Mwaipopo, Kipre Tchetche, Mrisho Ngassa, Zahoro Pazi, Khamis Mcha na George Odhiambo ‘Blackberry’ wakati washambuliaji ni Gaudence Mwaikimba, John Bocco ‘Adebayor’.
    Hii ni mara ya kwanza kwa Azam FC kucheza Kombe la Kagame, baada ya kushika nafasi ya pili katika msimu uliopita wa Ligi Kuu. Katika Kombe la Kagame mwaka huu, wenyeji Bara wataingiza timu tatu, Yanga ambao ni mabingwa watetezi, wakati Simba na Azam wanaingia kwa nafasi za uwakilishi.
    Wakati huo huo: Kahemele amesema kwamba, Azam FC imepanga kuifikisha klabu ya Simba kwenye Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), iliyo chini ya Mwenyekiti, Kamanda Mstaafu wa Polisi, kanda maalum Dar es Salaam, Alfred Tibaigana iwapo itaendelea na mpango wa kumuiba mchezaji wao, Jeba.
    Simba na Azam zinamgombea mchezaji huyo chipukizi, ambaye msimu uliopita alichezea Villa Squad Ligi Kuu kwa mkopo akitokea kwa wana Lamba Lamba, lakini Wekundu wa msimbazi wanasema kinda huyo hana mkataba na Azam. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC KAMBINI IJUMAA SHAMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry