• HABARI MPYA

    Tuesday, April 10, 2012

    PELE: NEYMAR NI BORA KULIKO MESSI

    Messi
    GWIJI wa soka Brazil, Pele amesema kwamba Neymar ni mwanasoka bora duniani zaidi ya nyota wa Barcelona, Lionel Messi, na amemtaka nyota huyo wa Argentina kwanza ampiku kinda huyo wa Santos kabla ya kushindajna naye.
    Mwanasoka huyo bora wa dunia mara tatu, akizungumza leo na Waandishi wa Habari katika hafla ya Santos, alisema hasikii aibu kuelezea uwezo mkubwa wa   Never kisoka.
    Babu huyo wa miaka 71 alisema kinda hyo yuko juu ya Messi katika orodha ya nyota wake wa soka wa duniani hivi sdasa.
    "Sasa kila mmoja anamzungumzia Messi, ni nyota. Lakini [kuwa bora daima] kwanza lazima awe bora zaidi ya Neymar," alisema.
    "Kwa sasa Messi ni tu ana uzoefu zaidi."
    Mbrazil huyo pia alipuuzia kuwepo kwa bifu kati yake na Diego Maradona, akisistiza kwamba hakuna kitu kama hcho baina yao.
    "Nyinyi [Waandishi] wakato wote mnasema mimi ni mpinzani wa Maradona, lakini si kweli. Sijawahi kuwa mpinzani wake, na alikuwa kiungo mshambuliaji babu kubwa," alisema gwiji huyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PELE: NEYMAR NI BORA KULIKO MESSI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top