// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); YANGA WAPINGA ADHABU ZA WACHEZAJI WAO, WAZIITA ZA UONEVU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE YANGA WAPINGA ADHABU ZA WACHEZAJI WAO, WAZIITA ZA UONEVU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, March 14, 2012

    YANGA WAPINGA ADHABU ZA WACHEZAJI WAO, WAZIITA ZA UONEVU


    KLABU ya Yanga imekata rufani Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ikipinga hatua ya Kamati ya Ligi ya shirikisho hilo kuwafungia wachezaji wake watano wakiwemo Stephano Mwasika na Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
    Juzi Kamati ya Ligi ya TFF iliyokutana Dar es Salaam ilitoa adhabu kwa wachezaji watano wa Yanga kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kudaiwa walimpiga mwamuzi wakati wa
    mchezo wa timu hiyo na Azam Jumamosi kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara uliomalizika kwa Yanga kufungwa mabao 3-1.
    Wachezaji hao ni Stephano Mwasika, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Jerry Tegete, Omega Seme na Nurdin Bakari, wanaodaiwa kumpiga mwamuzi Israel Nkongo kwenye mechi hiyo.
    Ofisa Habari wa Yanga, Luios Sendei alisema jana kuwa adhabu walizopewa wachezaji hao ni kubwa na zinaua vipaji vyao, hivyo wataomba kwa Kamati ya Nidhamu ya TFF kuwapunguzia
    adhabu hizo.
    Kulingana na Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, Cannavaro, amefungiwa mechi sita za Ligi Kuu na kupigwa faini ya Sh 500,000, baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwa kosa la
    kumshambulia mwamuzi Israel Nkongo kwenye mechi hiyo ya Yanga na Azam.
    “Wachezaji wengine wa Yanga walioadhibiwa kutokana na mechi hiyo ni Nurdin Bakari amefungiwa mechi tatu na faini ya Sh 500,000, Omega Seme amefungiwa mechi tatu na faini ya Sh 500,000, Jerryson Tegete amefungiwa miezi sita na faini ya Sh 500,000.
    “Stephano Mwasika amefungiwa mwaka mmoja na faini ya Sh milioni moja kwa kumpiga mwamuzi Nkongo. Adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu.
    “Kamati ya Ligi imempongeza Nahodha wa Yanga, Shadrack Nsajigwa na mshambuliaji wa timu hiyo Hamis Kiiza kwa kuwa mstari wa mbele kuzuia wenzao kumshambulia mwamuzi. Pia
    imempongeza kocha Kostadin Papic wa Yanga kwa kukemea vurugu zilizofanywa na wachezaji wake,” alisema.
    Hata hivyo akizungumzia hilo, Sendeu alisema wameomba radhi kwa tukio lililofanywa na wachezaji, hivyo TFF iwasaidie kwa kuwapunguzia adhabu.
    “Mwasika kwa muda mrefu alikuwa majeruhi, ndiyo ameanza kucheza, lakini Nurdin pia alikuwa majeruhi, tunaamini TFF itafikiria angalau kuwapunguzia adhabu. Ni kubwa sana na inaua vipaji vyao,” alisema.
    Kwa upande wake Wambura alikiri Yanga kuwasilisha barua TFF, ikidai wachezaji wake wameonewa katika mchezo huo.
    Wakati huohuo, Wambura alisema Kamati hiyo ya Ligi pia imetoa adhabu kwa Villa Squad ambayo imetozwa faini ya Sh 500,000 baada ya mashabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi dhidi ya Azam iliyochezwa Februari 15 mwaka huu Uwanja wa Chamazi.
    “Pia klabu hiyo imepigwa faini ya Sh 300,000 kwa kuchelewa uwanjani kwenye mechi namba 129 dhidi ya Mtibwa Sugar iliyochezwa Februari 19 mwaka huu Uwanja wa Manungu.
    Nayo Yanga imepigwa faini ya Sh 500,000 kutokana na mashabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi dhidi ya Azam,” alisema Wambura na kuongeza kuwa Yanga imepigwa faini ya Sh 500,000 baada ya wachezaji wake kuoneshwa kadi kuanzia tano kwenye mechi dhidi ya Azam.
     “Mchezaji Juma Mohamed wa Polisi Dodoma amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya Sh 500,000 baada ya kuwashambulia watazamaji kwa chupa ya maji katika mchezo kati ya timu
    yake na Villa Squad uliochezwa Februari 11 mwaka huu,” alisema
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA WAPINGA ADHABU ZA WACHEZAJI WAO, WAZIITA ZA UONEVU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top