Kikosi cha Yanga kilichotoa sare ya 1-1 na Zamalek |
KUNA
mechi nyingine katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara zina mvuto wa michuano
ya Afrika, kama Kombe la Shirikisho na Ligi ya Mabingwa michuano ambayo Yanga
wametolewa na Zamalek mwishoni mwa wiki.
Bila
shaka, hata mechi kati ya Azam FC na Yanga Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam inaweza kuwa tamu pengine kuliko hata ile mechi ya Simba na Kiyovu.
Yanga
inashuka dimbani kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi kumenyana na Azam, ikiwa ina
hasira nao ile mbaya.
Hasira
za Yanga zinatokana na nini? Kwanza wamefungwa na Zamalek na kutolewa kwenye
michuano ya Afrika mapema kama ilivyo kawaida yao.
Lakini
pili, Yanga imefungwa na Azam mara mbili mfululizo- kwanza kwenye mechi ya Ligi
Kuu 1-0 kwenye Ligi Kuu Septemba 18, mwaka jana Uwanja wa Taifa na baadaye kwenye
Kombe la Mapinduzi Januari, mwaka huu.
Lakini
yote tisa, 10 ni kwamba Yanga inataka kupoza machungu ya mashabiki wake baada
ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa- hivyo Jumamosi watataka kushinda kwa
lazima, licha ya ubora wa Azam wanoutambua.
Yanga
iliyorejea Jumatatu kutoka Cairo, inasifiwa kucheza soka ya kuvutia licha ya kufungwa
na Zamalek, jambo ambalo linawafanya mashabiki wa timu hiyom wawe na hamu kubwa
ya kuiona timu yao.
Mechi
ya Jumamosi itawakutanisha vinara wa mabao katika Ligi Kuu, John Bocco kwa upande
wa Azam anayeongoza kwa mabao yake 12 na Kenneth Asamoah kwa Yanga, anayefuatia
kwa mabao yake 10.
Lakini
pia itawakutanisha makipa wanaowania kumvua glavu Juma Kaseja katika timu ya
taifa ya Tanzania, Taifa Stars Mwadini Ally wa Azam na Shaaban Kado wa Yanga
ambao wote ni makipa wa akiba katika kikosi cha Mdenmark Jan Borge Poulsen.
Haruna
Hakizimana Fadhil Niyonzima kwa sasa unaweza kusema ndiye mchezaji bora zaidi
wa kigeni katika Ligi Kuu- lakini Azam pia ina viungo wazuri wazawa kama Salum
Abubakar ‘Sure Boy’, Abdi Kassim ‘Babbi’ na Jabir Aziz, ambao wote wanaifanya
mechi hiyo iwe na ‘quality’ za Afrika.
Kocha
Muingereza Stewart Hall, baada ya kutwaa Kombe la Mapinduzi Januari mwaka huu,
katika michuano iliyoshirikisha Simba na Yanga, tena akizifunga timu zote hizo,
ameweka bayana sasa anataka kufuta utawala wa vigogo hao na kwenye Ligi Kuu ya
Bara.
Lakini
kocha aliyekalia kuti kavu Yanga, Mserbia Kostadin Bozidar Papic hatahitaji
presha zaidi na dawa ya kuepuka hali hiyo ni ushindi tu Jumamosi.
Mambo
mengine yanayoifanya mechi hiyo iwe tamu ni kwamba Azam ina wachezaji ambao
misimu michache iliyopita walikuwa wanang’ara Yanga kama Mrisho Ngassa na Abdi
Kassim.
REKODI YA YANGA AZAM FC:
Septemba 18, 2011
Azam 1-0 Yanga
Machi 30, 2011
Yanga 2-1
Azam
Oktoba 24, 2010
Azam 0-0 Yanga
Machi 7, 2010
Yanga 2-1
Azam
Oktoba 17, 2009
Azam 1-1 Yanga
Aprili 8, 2009
Yanga 2-3
Azam FC
Oktoba 15, 2008
Azam FC 1-3
Yanga
0 comments:
Post a Comment