Xavi |
KIUNGO
wa Barcelona, Xavi amesema leo kwamba wachezaji wa klabu hiyo wanahofia kocha
Pep Guardiola ataamua kutosaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Ulaya.
“Hatuko
tayari kukataliwa na Guardiola. Tunatumai atabaki,”alisema nyota huyo wa
kimataifa wa Hispania.
“Guardiola
ni kielelezo muhimu katika mfumo wa Barca. Naona yuko vizuri, anafurahia. Anaendelea
kuwa mshindani kama ada, lakini uamuzi ni wake. Binafsi, nafikiri atasaini
mkataba."
Sintofahamu
inaendelea kuzingira mustakabali wa Guardiola, ambaye atamaliza mkataba wake
mwishoni mwa msimu nab ado hajaingia mkataba mpya baada ya kupiga kazi kwa
miaka mitatu na nusu Camp Nou.
Siku
moja baada ya kufikisha mabao 50 katika klabu hiyo, nyota wa Barca, Lionel
Messi alisema Jumatatu kwamba Guardiola alikuwa muhimu zaidi kwa klabu hiyo ya
Catalan zaidui yake (Messi).
0 comments:
Post a Comment