Yassin Mugabi |
MGOMO wa wachezaji katika Ligi Kuu ya Uganda , Bell Super
League umeingia katika siku ya pili leo, safari hii ukihusisha mechi kati ya
Proline na Water kwenye Uwanja wa Nakivubo jioni ya leo.
Wachezaji wa Ligi Kuu wametupa taulo zao Ijumaa wakitoa
madai kadhaa ikiwemo kulalamikia mfumo mzia wa Shirikisho la Soka Uganda (FUFA),
viwango vya mikataba na haki zao, jambo ambalo limesababisha mechi tatu
kutochezwa ndani ya siku mbili.
Kama ilivyokuwa katika mechi ya Bombo ambako Simba ilikipiga
na Express jana, ilibidi isimamishwe baada ya wachezaji saba wa Red Eagles kushindwa
kuendelea na mchezo kwa madai ni majeruhi, Water pia ilianza na wachezaji saba
dhidi ya 11 wa Proline, baada yaw engine kutotokea.
Dajkikam tisa ndani ya mchezo huo, Kasule Umar naye
akaanguka chini kwa majeruhi. Alitibiwa na watu wa huduma ya kwanza ili kurejea
uwanjani, lakini ikashindikana, huku akipigiwa makofi na watoto wa shule katika
mechi iliyohezwa kwenye Uwanja ‘mweupee’.
Kwa mujibu wa sheria za soka, refa alilazimika kuvunja mechi
hiyo kutokana na Water kubaki na wachezaji sita tu.
Watu wengine walisema Umar alidanganya kuumia, lakini kocha
wake, Charles Ayiekoh alimtetea.
“Si kweli,” alisema Ayiekoh na kuongeza; “Amekuwa
akisumbuliwa na tatizo la goti na alikosa mechi zetu mbili zilizopita,”alisema.
“Hivyo nilipofika hapa na kukuta wachezaji sita tu wamefika
kwa ajili ya mechi, ikabidi nimpigie simu yeye aje. Inauma, maunmivu yamemrudia.”
Wakati Umar anaanguka, kipa Yasin Mugabi alikuwa
amekwishawapa Proline bao la kuongoza dakika ya tatu kwa mpira wa adhabu.
Mechi nyingine kati ya KCC na Hoima-Busia na Maroons dhidi
ya Polisi, puia hazikuendelea.
Kampuni ya Ligi Kuu Uganda, USL itakutana na klabu za Ligi
Kuun Jumatatu kujaribu kutatua tatizo hilo.
0 comments:
Post a Comment