// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TUTARAJIE CLASSICO AU MOURINHO NA CHELSEA TENA? - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TUTARAJIE CLASSICO AU MOURINHO NA CHELSEA TENA? - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, March 16, 2012

    TUTARAJIE CLASSICO AU MOURINHO NA CHELSEA TENA?


    NYON, Uswisi
    MECHI kati Barcelona na Real Madrid “Clasico,”  Jose Mourinho kukutana tena na Chelsea au marudio ya fainali ya kwanza, misimu 20 iliyopita baina ya AC Milan na Marseille ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa katika droo ya mechi za  Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya inayopangwa leo mjini hapa.
    Droo la leo linalohusisha timu nane kama kawa kutoka nchi saba tofauti, linahusisha mabingwa sita wa zamani— wakiwemo Milan, Bayern Munich, Benfica na Marseille— pamoja na timu iliyowahi kutinga fainali, Chelsea na wakuzuka APOEL ya Cyprus .
    Barcelona na Madrid, na wakali wao wa mabao Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, watakuwa wapinzani wa kuogopewa ile mbaya hasa kufuatia kauli ya rais wa UEFA, Michel Platini kwamba timu hizo za Hispania zikikutana katika fainali itakuwa hatari tupu “bonge la fainali.”
    Barcelona ilitwaa taji la nne la Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, baada ya kuitoa  Madrid katika Nusu Fainali ambayo ilishuhudiwa kocha wa Madrid, Mourinho akifungiwa kuhusika katika mchezo wa marudiano kwa utovu wa nidhamu.
    Bado, mabingwa mara tisa wa michuano hiyo, Madrid wameimarika mno katika msimu huu wa pili chini ya kocha huyo Mreno, ambaye anaweza kuibuka kocha wa kwanza kutwaa mataji matatu ya Ligi ya Mabingwa akiwa na klabu tatu tofauti.
    Mourinho alitwaa taji hilo akiwa na FC Porto mwaka 2004 na Inter Milan 2010, lakini alishindwa kumpa taji hilo mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich katika miaka yake mitatu ya kupiga kazi London.
    Chini ya Mourinho, Inter iliifunga Chelsea katika hatua ya 16 bora miaka miwili iliyopita na safari yake ya kuelekea taji hilo inaweza kumpeleka tena Magharibi mwa London baada ya wakongwe Didier Drogba, John Terry na Frank Lampard kufanya kazi ya ziada na kuitoa timu matata Napoli juzi.
    “Watu hawawezi kuelewa kiasi gani naipenda Chelsea na ninafahamu ikiwa nitakutana nao kwenye Robo Fainali, watakuwa wapinzani wakubwa,” alisema Mourinho juzi baada ya Madrid kushinda kwa jumla ya mabao 5-2 dhidi ya CSKA Moscow. “Ningependa kucheza nao katika fainali.”
    Ushindi wa Chelsea unaihakikishia England kuendeleza rekodi yake ya kuwa nchi pekee iliyofululiza kufika Robo Fainali tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo mwaka 1997.
    Mechi za kwanza zitachezwa Machi 27 na 28, wakati marudiano yatakuwa Aprili 3 na 4.
    UEFA pia itataja leo tarehe za Nusu Fainali wakati fainali inafahamika itapigwa Mei 19 mjini Munich.
    Bayern inawania kuwa timu ya kwanza kuwania taji katika ardhi ya nyumbani tangu AS Roma ifungwe mwaka 1984 kwenye Uwanja wa Olympic dhidi ya Liverpool. Madrid pekee (1957) na Inter (1965) zilitwaa ubingwa huo wa Ulaya katika viwanja vyao.
    Pamoja na kwamba mwaka huu Ligi ya Mabingwa imekuwa haitabiriki, lakini Robo Fainali imetengeneza uwiano wa nguvu.
    Timu sita zimetwaa mataji 27 katika miaka 56, wakati Chelsea ilikaribia kutwaa katika fainali ya mwaka 2008 kwa mikwaju ya penalti dhidi ya Manchester United.
    Barcelona inaweza kuibuka klabu ya kwanza kutetea taji hilo ndani ya miaka 20, tangu enzi za michuano ya zamani, haijaingizwa kwenye mfumo huu mpya unaotumika sasa.
    Marseille walikuwa mabingwa wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa wakiifunga Milan 1-0 katika fainali mwaka 1993 kwenye Uwanja wa Olimpiki, Munich.
    Wafaransa hao sasa wanatinga Robo Fainali kwa mara ya kwanza tangu wakati huo.
    Droo la leo, linaweza pia kuzikutanisha timu zilizokutana kwenye fainali mwaka 1994, wakati Milan ilipoifunga Barcelona mabao 4-0 mjini Athens.
    APOEL wanataka kuleta hadithi ya Cinderella kwa kuwa timu ya kwanza ya Cyprus kufika hatua hii, kwa bajeti yao ya mishahara timu nzima ya dola za Kimarekani Milioni 13, ambayo haifikii mshahara anaopewa Mourinho pekee pale Madrid.
    Klabu hiyo kutoka jiji la Nicosia imefuzu Robo Fainali licha ya kufunga mabao machache tu, saba kama Barcelona na Bayern walivyofanya kwenye mechi zao moja moja zilizopita.
    APOEL imepigwa bao na Messi, ambaye rekodi yake ya mabao katika mashindano ya msimu huu ni 12 yakiwemo matano aliyofunga kwenye ushindi wa 7-1 dhidi ya Bayer Leverkusen wiki iliyopita na Mario Gomez, aliyefunga manne kwenye ushindi wa 7-0 dhidi ya FC Basel Jumanne na kufikisha mabao 10.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TUTARAJIE CLASSICO AU MOURINHO NA CHELSEA TENA? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top