|
CHELSEA mmeipata hiyo? Napoli, timu ya zamani ya Diego Armando Maradona imepiga mtu goli sita. Ikielekea kwenye
mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Chelsea katika hatua ya
16 Bora, Napoli imeichapa Cagliari mabao 6-3 jana, huo ukiwa ushindi wake wa
sita mfululizo kwenye mashindano yote.
Wakati huo huo, Inter Milan imeipiga Chievo Verona 2-0 kwa
mabao ya dakika za lala salama ya Walter Samuel na Diego Milito na kumaliza
nuksi la kutoshinda ndani ya mechi nane mfululizo.
Marek Hamsik, Paolo Cannavaro, Ezequiel Lavezzi, Walter
Gargano na Christian Maggio kila aliifungia bao Napoli, ambayo pia ilinufaika
na bao la wapinzani wao kujifunga, kupitia kwa Davide Astori.
Mshambuliaji wa Argentina, Joaquin Larrivey aliifungia mabao
matatu peke yake Cagliari.
Napoli sasa inashikana na Udinese katika nafasi ya nne, wakizidiwa
point inane na vinara wa Serie A, AC Milan, ambao leo wanaikaribisha Lecce. Inter
imepanda hadi nafasi ya sita ikizidiwa pointi 14.
0 comments:
Post a Comment