// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TENGA AWAPA VIDONGE VYAO YANGA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TENGA AWAPA VIDONGE VYAO YANGA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, March 16, 2012

    TENGA AWAPA VIDONGE VYAO YANGA


    SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) limesema adhabu walizopewa wachezaji wa klabu ya soka ya Yanga ni sahihi kwani kumpiga mwamuzi ni utovu wa nidhamu.
    Hatua hiyo inafuatia Yanga kulalamikia adhabu ya vifungo na faini waliyopewa wachezaji wake watano kutokana na kumpiga mwamuzi Israel Nkongo mmwishoni mwa wiki iliyopita wakati Yanga ilipocheza na Azam Fc katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwewnye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam .
     Rais wa TFF Leodger Tenga alisema wachezaji hao waliadhibiwa kwa mujibu wa sheria na Kanuni za soka na mchezaji yoyote atakayeonyesha vitendo vya utovu wa nidhamu ataadhibiwa kwa mujibu wa kanuni.
    “Wachezaji kumpiga mwamuzi si tu kinyume cha sheria ni utovu wa nidhamu…haya mambo yalikuwa zamani lakini kwa sasa mambo hayo yanatakiwa kufanywa katika mechi za mchangani lakini si kwa wachezaji ambao tunateghemea siku moja wakacheze soka la kulipwa nje ya nchi,”Alisema Tenga.
    Kama hiyo haitoshi, Tenga alishangazwa na kitendo cha wazee wa klabu ya Yanga kutoa malalamiko yao na kutishia mamboi kadhaa kuhusiana na adhabu waliuzopewa wachezaji wa timu hiyo na kusema kuwa walipaswa kukemea vitendo vya utovu wa nidhamu kwani msimamo walioutoa inaonyesha wanaunga mkono wachezaji wa Yanga.
    “Utu Uzima Dawa si Sumu…haiwezekani wachezaji watende vile halafu mzee asikemee kwani kwa kufanya hivyo inaondoa kauli mbiu ya Yanga DAIMA MBELE NYUMA MWIKO…lakini hilo halipo kwao,”Aliongeza Tenga.
    Katika hatua nyinmgine, Tenga amesema kuanzia sasa uharibifu wowote utakaotokea kwenye uwanja wa Taifa klabu husika italazimika kulipa gharama ya shilinmgi milioni 10 iliyoelekezwa na Serikali.
    Tenga alisema Serikali ina haki ya kutoza faini hiyo kutokana na Watanzania kushindwa kuonyesha ustaarabu wa kuuthamini uwanja huo uliojengwa na Serikali na badala yake wamekuwa wakiuharibu kutokana na vurugu zisizo na maana ambazo hufanywa na mashabiki wa baadhi ya vilabu.
    “Ni sawa kwa Serikali kutangaza faini kwa uharibifu utakaotokea kwenye Uwanja wa Taifa lakini pia ifike mahali viongozi wa vilabu husika kuwaelimisha wanachama na wapenzi wao kuacha kufanya mambo yasiyo ya kistaarabu ndani ya uwanja kwani ni vigumu kwa TFF pekee kusimamia suala la ulinzi ama uangalizi wa uwanja,”alisema Tenga.
    Aidha, Tenga aliongeza mpira ni burudani na furaha hivyo mambo ya kihuni yanayofanywa na baadhi ya mashabiki hayaendani na lengo la michezo na kwa mwendo huo itafikia wakati makampuni yataacha kudhamini mchezo huo na matokeo yake kuendelea kurudisha nyuma kiwango cha mchezo huo.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TENGA AWAPA VIDONGE VYAO YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top