// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SSENTONGO ANATISHA KWA MABAO UGANDA, ATUPIA TENA MAWILI URA IKIUA 4-1 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SSENTONGO ANATISHA KWA MABAO UGANDA, ATUPIA TENA MAWILI URA IKIUA 4-1 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 10, 2012

    SSENTONGO ANATISHA KWA MABAO UGANDA, ATUPIA TENA MAWILI URA IKIUA 4-1


    Ssentongo Mabao

    HAWEZI kuacha kufunga mabao na URA haiwezi kuacha kushinda katika Ligi Kuu ua Uganda, Bell Super League, japokuwa mechi nyingine tatu zimeshindikana kufanyika kutokana na wachezaji kugoma wakidai haki zao.
    Si mwingine, alikuwa ni mshambuliaji wa zamani waq, Robert Ssentongo alipoipachikia mabao mawili URA katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Bidco.
    Wakusanya kodi hao wa Uganda, wamekuwa katika wiki tatu nzuri mno, kwani pia wamesonga mbele katika Ligi ya Mabingwa.
    Mshambuliaji wa The Cranes, Ssentongo aliyefunga mawili pia katika ushindi wa 4-1 kwenye mechi yao iliyopita ya ligi dhidi ya Fire Masters, alipiga mabao hayo jana katika dakika za 11 na 12.
    Moses Feni alifunga la kwanza timu hiyo ya Alex Isabirye, ambayo inaendelea kuwa juu ya Bunnamwaya inayoshika nafasi ya pili kwa pointi 37 dakika ya 22 kabla ya Nyanzi Umari kuifungia Bidcodakika nane baadaye.
    Lakini Ssentongo alifunga kabla ya mapumziko na linguine dakika ya 61.  Bao la Hamis Kitagenda dakika nane kabla ya filimbi ya mwisho lilihitimisha karamu ya mabao ya URA dhidi ya kikosi cha Richard Makumbi, Bidco ambacho kinaporomoka hadi nafasi ya 11 kwa pointi zake 20.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SSENTONGO ANATISHA KWA MABAO UGANDA, ATUPIA TENA MAWILI URA IKIUA 4-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top