Kikosi cha Simba |
Kikosi cha Yanga |
Simba sasa wana pointi 44, baada ya kucheza mechi 20 wakati Azam ipo nafasi ya pili kwa pointi zake 41 baada ya kucheza mechi 20 pia, wakati Yanga iliyoifunga African Lyon 1-0 inashika nafasi ya tatu kwa pointi zake 40, ingawa imecheza mechi 19.
Bao pekee la Simba kwenye mchezo huo, lilitiwa kimiani na kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Mutesa Patrick Mafisango. Bao la Yanga lilikuwa kama la kujifunga, kwani beki Hamisi Yussuf aliokoa mpira ukambabatiza kiungo Kiggi Makassy na kutinga nyavuni.
Azam itashuka dimbani Jumapili kucheza na Ruvu Shooting Uwanja wa Azam, Chamazi, siku ambayo Simba watakuwa wakimenyana na Mtibwa Sugar Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Jumamosi Yanga itacheza na Villa Squad Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati
0 comments:
Post a Comment