MWENYEKITI wa Zamalek, Mamdouh Abbas ametangaza kwamba mechi
ijayo dhidi ya wapinzani wao wa jadi, Al Ahly itafanyika baadaye mwezi huu.
Abbas ameaimbia SuperSport kwamba amekubaliana na Mwenyekiti
wa Al Ahly, Hassan Hamdy na ofa hiyo imekubaliwa.
Inayopaswa kutuunga mkono ni Wizira ya Mambo ya Ndani, lakini
ninaamini watauidhinisha mchezo huu. Wakifanya hivyo, mechi hiyo itachezwa kati
ya Machi ya 23 na 27 " alisema.
Katika mchezo huo, kila timu itavaa jezi za mpinzani wake
ili kuonyesha umoja, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya upinzani
wa timu hizo.
Mechi hii inakuja siku chache baada ya kutokea janga la
mauaji ya watu 74 lililotokea kwenye mji wa Port Said wakati wa mechi ya Ligi
Kuu ya Misri kati ya Al Masry na Al Ahly.
Je, iko siku katika kujenga umoja, wapinzani wa jadi wa Tanzania nao, Simba na Yanga
zitabadilishana jezi? Lakini je, mashabiki tu Misri watakubali wazo hilo? Tusubiri
tuone.
0 comments:
Post a Comment