Felix Sunzu kushoto akishangilia na Patrick Mafisango na Emanuel Okwi |
MECHI ya Kombe la Shirikisho Afrika, kati ya Simba SC na Kiyovu
ya Rwanda imeingiza kiasi cha 208,843,000.00, imeelezwa.
Mechi hiyo iliyosimamiwa na kampuni ya Prime Time Promotions
ya Dar es Salaam, ilichezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na SImba
ilishinda mabao 2-1, yote yakitiwa kimiani na Felix Sunzu.
Simba imeingia Raundi ya Pili ya Kombe la Shirikisho kwa
ushindi wa jumla wa mabao 3-2, kufuatia sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza mjini
Kigali.
Hata hivyo, mapato hayo hayafui dafu kwa mapato ya mechi ya
kwanza ya Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na Zamalek
ya Misiri, ambayo iliingiza Sh 286, 695.000,00 wiki tatu zilizopita kwenye
Uwanja huo huo.
Katika mchezo, timu hizo zilitoka sare ya 1-1 Yanga
ikitangulipa kupata bao lililofungwa na Hamisi Kiiza na Zamalek kusawzisha
kupitia kwa Amr Zaki.
0 comments:
Post a Comment