// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SHOMARI SALUM KAPOMBE: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SHOMARI SALUM KAPOMBE: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 17, 2012

    SHOMARI SALUM KAPOMBE:


    KWA muda mrefu miaka ya karibuni mabeki wa pembeni imekuwa ni tatizo nchini, na ndio maana Nsajigwa Shadrack amekosa upinzani kwenye beki ya kulia tangu mwaka 2006.
    Haruna Shamte alijaribu kutaka kupora namba ya Nsajigwa,lakini akachemsha ila sasa Shomari Salum Kapombe kwa kasi anayokuja nayo anaelekea kuleta mapinduzi ya kweli.
    Huyu ni beki chipukizi wa timu ya taifa ya Tanzania na Simba, anayemudu kucheza pia na nafasi za kiungo ambaye,anainukia vizuri kisoka.
    “Ninamudu kucheza nafasi zote pale kocha atakaponipanga kwani mpira upo kwenye damu yangu,” anasema Kapombe katika mahojiano maalum na DIMBA yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
    Ni mchezaji chipukizi ambaye anacheza beki kulia na kiungo, kutokana na uhodari wake uwanjani, jina hili limekuwa maarufu sana, kwani katika kikosi cha timu ya vijana chini ya miaka 23  na hata ile ya wakutwa, mchezaji huyo hakosekani, na ndio maana amejizolea umaarufu mkubwa sana.Nyota ya Kapombe ilianza kung’ara pale alipoitwa kwa mara ya kwanza   katika kikosi cha U-23 kilichokuwa kikiwania kufuzu michuano ya Olimpiki na Mataifa ya Afrika, na kwenye mechi kadhaa za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara iliyomalizika Novemba 3, akiwa na vinara wa ligi hiyo, Simba, hali iliyomfanya kocha wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ Jan Borge Poulsen avutiwe naye.
    Baada ya kuvutiwa na soka ya mchezaji huyo, Poulsen alimwita katika kikosi chake kilichokuwa kikiwania kupangwa kwenye makundi ya kufuzu Fainali za   Kombe la Dunia, dhidi ya Chad, mechi hiyo ilichezwa  jijini Nd’jamena, Novemba 11 na kurudiana siku nne baadaye jijini Dar es Salaam, ambapo Stars walifanikiwa kuwaondoa Chad.
    Kutokana na nahodha wa timu ya taifa, Taifa Stars, Nsajigwa Shedrack kuwa majeruhi, kinda huyo alikuwa akicheza nafasi ya mkongwe huyo, beki ya kulia.
    Alicheza mechi zote dhidi ya Chad na michuano ya Kombe la Tusker Challenge iliyomalizika mwezi huu, ambapo timu yake ya Tanzania Bara ilishika nafasi ya nne.
    Katika mahojiano maalumu na DIMBA Kapombe mwenye historia ndefu katika medani ya soka, licha ya kuwa na umri mdogo, baada ya kutua Simba msimu huu, amefanikiwa kupigana vilivyo na kula sahani moja na nyota kadhaa wakongwe na wa kimataifa na kufanikiwa kucheza mechi karibu zote za mzunguko wa kwanza.
    Kapombe alizaliwa Januari 28 mwaka 1992, alihitimu elimu yake ya msingi mwaka 2006 katika shule ya msingi Morogoro kabla ya kumaliza elimu yake ya sekondari mwaka 2010 katika shule ya Lupamba mjini Morogoro.
    Ni mtoto pekee ya kiume katika familia yam zee Salum yenye watoto watatu, wakike wawili, yeye akiwa kitinda mimba.
    “Mpira upo kwenye damu yangu, kwani nilianza kuupenda tangu utotoni, na hivyo nikaanza kucheza mechi mbalimbali za  mitaani ambako pia nilikuwa navuma sana,” anasema Kapombe
    .Anasema alianza kujitambua kama mwanasoka tangu akiwa darasa la tatu, kipindi hicho alikuwa kwenye kituo cha Morogoro Youth Academy, ambapo pia alikuwa akishiriki michuano mbalimbali ambayo ilikuwa ikiandaliwa na kituo hichoKapombe anasema pia aliwahi kucheza na timu ya watoto wanaookota miopira kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro ambayo ilikuwa ikiitwa  Jamhuri Ball Boys.
    “Mimi nilikuwa ni muokota mipira pale Uwanjawa Jamhuri mjini Morogoro, hapo ndipo utakapogundua kwamba mpira upo kwenye damu yangu, hapo ndipo ikaundwa timu yetu sisi watoto waokota mipira ambayo iliitwa Jamhuri Ball Boys.
    “Timu nyingine ambazo nilichezea ni  Mafiga Kids, Santos Fc, Jamhuri Ball Boys mpaka nilipokuja kuonekana na kituo cha Moro Youth Academy, nilikuwa najituma sana nikijua fika ipo siku nitakuja kufika mbali sana katika soka,” anasema.
    Anasema katika timu ya  Jamhuri Ball Boys, U-14,alikuwa ni nahodha wa timu hiyo katika michuano ya Winome Cup  na  michuano ya Serve Access Games ambapo aling’ara sana.
    Kapombe anasema mtu ambaye hata kuja kumsahau katika maisha yake ya soka ni kocha wake  Yahya Belin, aliyekuwa akikinoa kikosi cha  Jamhuri Ball Boys, kwani ndiye aliyemsaidia kuinua kipaji chake.
    Anasema kocha  Belin, alikuwa akimsihi acheze namba tofauti tofati uwanjani, ili siku ikitokea mmoja wa wachezaji akiumia basi acheze yeye nafasi hiyo kuliko kumtegemea mchezaji mmoja katika nafasi Fulani hivyo yeye akiwa kiraka.
    Akiwa katika kituo hicho cha Moro Youth, baadaye alipanda hadi kikosi cha U-17 cha kituo hicho, ambako aliweza kuchaguliwa kuwa nahodha wa timu ya mkoa wa Morogoro iliyoshiriki michuano ya Copa Coca-Cola 2008, wakati huo akiwa na miaka 16.
    Anasema katika mashindano hayo walitolewa hatua ya robo fainali na Kigoma ambayo ilikuja kuwa mabingwa.
    Kapombe anasema uhodari mkubwa aliokuwa akiuonyesha katika michuano hiyo faida yake alikuja kuiona baadaye baada kuchaguliwa wachezaji nyota wakati huo ilikuwa ni mwaka 2008, na walitakiwa kwenda nchini Brazil, katika mkoa wa Morogoro walichaguliwa wawili yeye pamoja na Zahoro Zeiran.
    Baada ya kumalizika kwa michuano hiyo, Kapombe anasema alirudi katika kituo chake cha Morogoro ambako alijiunga na kikosi cha timu B cha Polisi Dodoma mwaka 2007, ambapo 2009 alipandishwa timu ya wakubwa.
    Kapombe anasema baada ya timu ya Polisi Moro kushuka daraja alikuwa akiitumikia timu hiyo katika mashindano ya Ligi Daraja la Kwanza.
    “Nakumbuka siku hiyo tulikuwa tunacheza na Arusha, katika mchezo huo kocha Jamhuri Kikwelu ‘Julio’ alikuwepo, hivyo alivutiwa na uwezo wangu na kunichagua katika timu ya taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 23.
    Anaongeza kuwa akiwa katika kikosi cha timu ya vijana alikuwa akiongeza bidii kila kukicha, na alijituma zaidi katika michuano ya kimataifa ya All African Games na Olimpiki ambapo aliweza kucheza mechi zote, nyumbani na ugenini, ikiwemo na timu za Cameroon, Nigeria na Uganda, hali ambayo ilizidi kumuongezeav uwezo zaidi na kujiamini.
    “Nashukuru Mungu Simba walivutiwa na uwezo wangu, hivyo msimu huu walinisajili katika kikosi chao, ambapo nimezidi kung’ara zaidi na hivyo kuwavutia makocha wangu wa Simba na wale wa timu za taifa.

    Anasema, baada ya kujiunga na Wekundu hao, furaha yake ilizidi pale alipokabidhiwa jezi namba 15 na kuwa miongoni mwa wachezaji 18 wa kikosi cha kwanza cha kutumainiwa cha aliyekuwa Kocha Mganda, Moses Basena.
    Kapombe anasema anafuraha zaidi kwani kocha wa Simba wakati huo, Mganda Moses Basena alivutiwa naye na hivyo akamchagua katika kikosi cha kwanza, hali ambayo anasema imempa changamoto kubwa katika maisha yake ya soka.
    “Kwanza nimecheza mechi zote 13 za mzunguko wa kwanza za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, hivyo inaonyesha kabisa uwezo wangu upo juu sana,” anasema.

    Jambo ambalo Kapombe anasema hata kuja kusahau katika maisha yake, ni mwaka 2002 alipofiwa na mama yake mzazi, Bi.Ester Shomari.
    “Kwakweli kila nikikumbuka huwa nalia sana, kwani alikuwa ni kipenzi change, ikizingatiwa mimi nilikuwa ni kitinda mimba wake,” anasema.
    Kapombe analishauri Shirikisho la SokaTanzania (TFF), kuwa na shule za michezo nyingi ili kukuza vipaji vya watoto.
    “Shule za michezo zinasaidia sana kwani kuna watoto wengi sana ambao wanavipaji, lakini hawana pa kuvionyesha,” anasema.

    WASIFU WAKE:
    JINA KAMILI: Shomari Salum Kapombe.
    KUZALIWA: Januari 28, 1992 (Miaka 19)
    ALIPOZALIWA: Morogoro.
    KLABU YAKE: Simba
    Mwaka          Klabu
    2007-2009     Polisi Dodoma
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SHOMARI SALUM KAPOMBE: Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top