// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SERIKALI YAZIDI KUIKOMALIA TFF UHARIBIFU WA VITI UWANJA WA TAIFA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SERIKALI YAZIDI KUIKOMALIA TFF UHARIBIFU WA VITI UWANJA WA TAIFA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, March 15, 2012

    SERIKALI YAZIDI KUIKOMALIA TFF UHARIBIFU WA VITI UWANJA WA TAIFA


    KUANZIA sasa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) litawajibika kulipa kiasi cha shilingi milioni 10 kwa uharibifu wa idadi yoyote ya viti utakofanywa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
    Hatua hiyo inafuatia kukithiri kwa uharibifu wa viti hivyo ambao umekuwa ukifanywa na mashabiki wa soka hapa nchini na hasa wa Vilabu vya Simba na Yanga. 
    Akizungumza  kwa niaba ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, mkurugenzi wa Idara ya Michezo nchini Leonard Thadeo alisema kwamba lengo la kufanya hivyo ni kudhibiti vitendo vya uharibifu wa viti katika Uwanja huo.
     Allisema fedha hizo zitalipwa bila kujali idadi ya viti hata kiwe kimoja au kumi kwani serikali imesikitishwa na kitendo cha muendelezo wa vurugu kwenye uwanja huo kwani kinawadhalilisha wanamichezo wote wa Tanzania na jumuiya ya Kimataifa. 
    Thadeo aliongeza kuwa uharibifu huo umekuwa ukifanyika mara kwa mara na serikali imekuwa ikilazimika kufanya matengenezo bila kuwahusisha wadau wengine lakini inaonekana kujengeka kuwa tabia miongoni mwa baadhi ya mashabiki hatua ambayo haiwezi kuvumilika. 
    “Inasikitisha kuona hata baadhi ya viongozi wa vilabu vyetu hawatambui kuwa wanawajibu wa msingi kama viongozi kuwaelimisha wanachama  na wapenzi wa vilabu vyao kuacha uharibifu badala yake wanadai kuwa viti vingi viliharibika,kaharibu nani? alihoji Thadeo. 
    Alisema sasa hivi dunia ni sawa na kijiji na wakati mataifa mengine yalikuwa yameanza kuisifia Tanzania kwa kujenda Uwanja wa kisasa na wa kimataifa, kudumisha amani na kutekeleza mambo kistaarabu, lakini vurugu hizo zinaweza kutia doa sifa zote hizo. 
     “Viongozi tutambue wajibu wetu kwa tunaowaongoza na wizara haitasita kufunga uwanja endapo tabia hiyo itaendelea...ili tusifikie hatua hiyo, tunawaomba wapendamichezo na Watanzania wote tushirikiane, tuhamasishane na kuelimishana kushangilia timu zetu kwa amani na utulivu,”Aliongeza Thadeo. 
    Hivi karibuni Serikali ilitaka TFF kulipa jumla ya shilingi milioni kumi kufuatia mashabiki kuahribu viti katika mechi ilizozihusisha timu za Simba na Yanga kwa nyakati tofauti ambapo kulitokea uharibifu wa viti ulioafanywa na mashabiki wa timu hizo. 
    Kufuatia hali hiyo TFF iliamua kuikata Simba shilingi milioni tano kwa madai kuwa mashabiki wake walifanya uharibifu huo katika mechi yao dhidi ya Kiyovu ya Rwanda kabla ya kuikata Yanga kiasi kama hicho kutokana na uharibifu uliofanywa katika mechi yao ya ligi kuu dhidi ya Azam.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SERIKALI YAZIDI KUIKOMALIA TFF UHARIBIFU WA VITI UWANJA WA TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top