Geoffrey Bonny wa Yanga mbele na Abdi Kassim wa Azam katika iliyotawaliwa na vurugu baina ya timu hizo |
SHIRIKISHO
Soka Tanzania (TFF) leo limepokea barua kutoka Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo juu uharibifu uliofanyika kutokana na vurugu za washabiki
wa Yanga kwenye mechi dhidi ya Azam.
Kwa
mujibu wa tathmini ya Serikali, katika vurugu hizo kwenye mechi hiyo ya Ligi
Kuu ya Vodacom iliyochezwa Machi 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
jumla ya viti 119 viliharibiwa. Gharama za uharibifu huo ni sh. milioni 5
ambazo Serikali imeagiza zilipwe mara moja.
Kwa
vile washabiki wa Yanga ndiyo waliohusika na vurugu na uharibifu huo, gharama
hizo zitabebwa na klabu hiyo ili Serikali iweze kufanya ukarabati haraka.
TFF
inarudia tena kulaani na kukemea vurugu zinazofanywa na washabiki viwanjani na
kusababisha usumbufu, uvunjifu wa amani na uharibifu wa vifaa hasa kutokana na ukweli kuwa mpira wa miguu
ni mchezo wa burudani.
Tunapenda
kuwakumbusha washabiki na klabu kuwa vitendo hivyo si vya kistaarabu, hivyo
havikubaliki katika mpira wa miguu, na TFF haitasita kuchukua hatua kali kwa wahusika
iwapo vitaendelea kutokea viwanjani.
0 comments:
Post a Comment