// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); RIBERY AWAONYA BAYERN, MARSEILLE SI WA KUBEZA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE RIBERY AWAONYA BAYERN, MARSEILLE SI WA KUBEZA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 17, 2012

    RIBERY AWAONYA BAYERN, MARSEILLE SI WA KUBEZA


    Ribery
    NAHODHA wa Bayern Munich, Philipp Lahm amefurahia kuziepuka bunduki kubwa za Hispania katika droo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopangwa jana– lakini yeyote kutoka timu hiyo ya Bavaria anahitaji kuelewa kwamba ili kuwajua vizuri wapinzani waliopangiwa, Olympique Marseille, amuulize Franck Ribery pekee.
    Mshambuliaji huyo wa Ufaransa alidumu kwa misimu miwili Stade Vélodrome, kutoka 2005 hadi 2007, na anaufahamu vema ugumu wanaouelekea Bayern katika mechi ya kwanza mjini Marseille Machi 28, 2011.
    “Hii si rahisi,”alisema Ribery alipozungumza na Uefa.com. "Kwa  Marseille itakuwa kimbembe. Watu wanapenda soka na mashabiki 60 000 watakuwa dhidi yetu."
    Akizungumzia Bayern kupangwa na OM, Lahm aliita "droo yenye akili ", akisema: "Nilisema itakuwa vema kuwaepuka Barcelona na Real, ndio maana tunaweza kufurahia."
    Bado hakuwa sahihi kuamini mabingwa hao wa mwaka 1993 ni wepesi licha ya wiki hii kutoka kuwang’oa Inter Milan na waliwapiga nyumbani na ugenini vinara wa Bundesliga, Borussia Dortmund katika hatua ya makundi.
    “Marseille ni hatari. Wameitoa Inter na waliifunga mara mbili Dortmund,"alisema. "Ni ahueni ndogo kwamba, tunaanzia ugenini."
    Kwa Marseille, mechi ya pili Aprili 3 itawarudisha Munich, jiji ambalo walishinda fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka 1993, katika maskani ya zamani ya Bayern, Uwanja wa Olympia.
    Ndoto za Bayern msimu huu ni kucheza mechi ya mwisho katika Uwanja wao wa nyumbani bna kocha wa Marseille, Didier Deschamps alisema inaweza hii "inaweza kuwa ya kuvutia kwa wapinzani wetu" kupangiwa timu ya Ligue 1 katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa tangu kampeni ya 1992/93.
    “Ni ngumu, wako imara sana,"alisema Deschamps, Nahodha wa kikosi cha Marseille mwaka 1993. "Kulikuwa kuna klabu mbili za Hispania, Real na Barcelona, lakini nafikiri kwamba Bayern ni timu inayofuatia ubora wao.
    Wana wachezaji wa ngvu na wenye kushambulia sana kama Ribery, [Arjen] Robben, [Thomas] Muller na [Mario] Gomez. Wana kipa wa kimataifa, [Manuel] Neuer, [Bastian] Schweinsteiger kwenye kiungo na Lahm na [OM kinda la Daniel] van Buyten katika beki nne. Ni wagumu sana."
    Bayern iliifunga timu nyingine ya Ufaransa, Olympique Lyonnais nyumbani na ugenini katika Nusu Fainali miaka miwili iliyopita, lakini Deschamps anaamini wamekusdanya uzoefu mkubwa msimu huu, ikiwemo ushindi dhidi ya Dortmund.
    “Lazima tuamini, vyovyote. Ni kweli tumewafunga Dortmund mara mbili, hata kama haikuwa rahisi. Wana pointi tano zaidi ya Bayern [kwenye Bundesliga], lakini Dortmund walijiandaa kwa Ligi ya mabingwa mwaka huu. Bayern ni hivyo pia. Tutapigana kwa uwezo wetu wote kaa tulivyofanya dhidi ya Inter."
    Japo ni rahisi kutabiri mshindi wa Robo Fainali kati ya Real Madrid na APOEL, lakini Mwenyekiti wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge amesema si vema kuangalia mbali zaidi.
    "Ni vema kwetu kutofikiria uwezekano wa kukutana na Real kwenye Nusu Fainali. Lengo letu ni kufika Nusu Fainali, ni wazi, lakini lazima tupige hatua ya kwanza kabla ya hatua ya pili. Mtazamo wetu kamili unatakiwa kuwa kwa Marseille."
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RIBERY AWAONYA BAYERN, MARSEILLE SI WA KUBEZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top