Manny Pacquiao kulia akipigana na Mmarekani Shane Mosley Mei 7, mwaka jana. |
MAOFISA Kodi wa Philippine, wamemfungulia malalamiko ya uhalifu
bingwa wa ndondi na Mbunge ambaye anahusika katika kutunga sheria, Manny
Pacquiao kwa kushindwa kuwasilisha makabrasha uili kufanyiwa uchunguzi ulipaji
wake wa kodi.
Waendesha mashitaka wataamua kama kuna ushahidi wa kutosha
ili kupeleka suaal hilo mahakamani, ambako Pacquiao anaweza kutupwa jela kwa
miaka miwili iwapo atakuwa na hatia.
Mkurugenzi wa Idara ya Mapato ya Ndani, Rozil Lozares amesema
kwamba malalamiko yalifunguliwa Machi 1, baada ya Pacquiao kushindwa
kuwasilisha makabrasha licha ya kupelekewa taarifa mara tatu.
Alisema juzi kwamba taarifa za kodi za Pacquiao mwaka 2010 zina
utata na ndizo waataka kuzifanyia uchunguzi, lakini yeye anakwepa.
Pacquiao ambaye jarida la Forbes Magazine mwaka jana lilimtaja
kama mwanamichezo anayeshika nafasi ya 24 duniani kwa utajiri, alipopigiwa simu
ili kujibu tuhuma hizo, ilikuwa inaita bila majibu.
0 comments:
Post a Comment