KLABU ya Sofapaka imeifunga Rangers mabao 2-1 katika mechi
kali iliyofanyika kwenye Uwanja wa Nyayo jana.
Sofapaka ilipata bao la kwanza dakika ya 10, wakati Abdallah
Juma alipofunga kwa mpira wa adhabu kutoka umbali wa mita 30, ambao ulimshinda
kipa wa Rangers, Victor Omondi na bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Rangers ilisawazisha dakika ya 57, wakati Michael Ochieng alipofunga
bonge la bao baada ya kuwatoka mabeki wawili kabla ya kumtungua kipa wa Sofapaka,
Duncan Ochieng.
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga, John Barasa aliifungia
Sofapaka bao la ushindi kwa mkwaju wa penalti baada ya beki wa Rangers
kumkwatua kwenye boksi Robert Binja aliyetokea benchi na refa akaamuru adhabu
hiyo, iliyotumiwa vyema na mkongwe.
0 comments:
Post a Comment