Neymar |
KINDA la Kibrazil, Neymar limepiga mabao matatu peke yake wakati
Santos ikiitandika Internacional 3-1 katika mechi ya wapinzani wa jadi Brazil,
hatua ya makundi ya Copa Libertadores usiku wa jana, wakati Fluminese iliichapa
Boca Juniors 2-1 na kuvunja rekodi ya klabu hiyo ya Argentina kutofungwa kwenye
mechi 36 katika mashindano yote.
Hat-trick ya Neymar inawapa mabingwa watetezi, Santos
ushidni wa kwanza katika mashindano hayo mwaka huu na kuipeleka klabu hiyo
katika nafasi ya pili kwenye Kundi la 1 kwa pointi zake tatu kwenye mechi mbili.
Katika Kundi la 4 mjini Buenos Aires, kiungo wa zamani wa Chelsea
na Ureno, Deco alimtengenezea bao la kwanza Fred aliloifungia Fluminese dakika
ya 10 na kufunga la ushindi dakika ya 55, baada ya Leandro Somoza kuisawazishia
Boca dakika mbili baada ya mapumziko.
Matokeo hayo yanaifanya Fluminense kufikisha pointi sita
kwenye Kundi la 4, wakati Boca ina pointi moja tu katika nafasi ya tatu.
0 comments:
Post a Comment