KIKAO
cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kilichokutana leo Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam kimeamua Mkutano Mkuu wa mwaka ufanyike mwsihoni mwa
mwezi Aprili.
Mkutano
huo, ambao ulishindwa kufanyika mwaka jana kwa mujibu wa Katiba, utajadili ambo
mengi ikiwemo suala la kampuni ya Klabu za Ligi Kuu, uanachama wa mikoa mipiya,
ambayo ni Katavi, Njombe, Geita, Simiu.
Aidha,
Mkutano huo unatarajiwa kujadili pia taarifa ya mapato na matumizi ya shirikisho
pamoja na Uchaguzi Mkuu, utakaofanyika mwsihoni mwa mwaka.
0 comments:
Post a Comment