MWANDISHI mwandamizi wa habari za michezo nchini, Samson Mbega aliyefariki dunia asubuhi ya jana, anatarajiwa kuzikwa kesho kwao Kisarawe, mkoani Pwani.
Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa marehemu, Mawazo Lusonzo ni kwamba msiba upo nyumbani kwa marehemu, nyuma ya kota za Temeke mwisho eneo la Pile Bar.
Ndugu wadau, waandishi wa habari naomba tujitokeze kwa wingi kumsindikiza ndugu yetu katika safari yake ya mwisho. Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu. Amin.
0 comments:
Post a Comment