// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MASIKINI ABIDAL, INAWEZA KUWA SOKA NDIO BASI TENA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MASIKINI ABIDAL, INAWEZA KUWA SOKA NDIO BASI TENA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, March 15, 2012

    MASIKINI ABIDAL, INAWEZA KUWA SOKA NDIO BASI TENA


    Abidal
    BILBAO, Hispania
    BEKI wa Barcelona, Eric Abidal ameingia katika wakati mgumu juu ya mustakabali wake kisoka baada ya leo kutangazwa kwamba anatakiwa kufanyiwa operesheni ya ini, karibu mwaka mwaka mmoja tangu afanyiwe operesheni nyingine kama hiyo.
    Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 32, anayecheza beki ya kushoto alifanyiwa upasuaji Machi 17, mwaka 2011, lakini alirejea kumalizia msimu na amekuwa akiendelea vizuri tangu wakati huo.
    Kwa heshima, Abidal aliteuliwa kunyanyua Kombe la nne la Ligi ya Mabingwa, baada ya klabu hiyo kulitwaa kwenye Uwanja wa Wembley baada ya kuiwezesha Barcelona kuifunga Manchester United mabao 3-1 kwenye fainali Mei mwaka jana.
    Abidal amekuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha mabingwa hao wa Hispania na Ulaya kwa msimu wote huu na amekuwa akiwavutia wachezaji wenzake, lakini walipigwa butwaa wakati kocha Pep Guardiola alipowapasulia habari kabla ya mazoezi kwamba anatakiwa kufanyiwa upasuaji.
    Habari hizo zinamaanisha kwamba Abidal hata nafasi yake ya kucheza michuano ya Euro mwaka huu huko Poland na Ukraine kuanzia Juni 8 hadi Julai katika kikosi cha Ufaransa iko shakani.
    Abidal amekuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza cha Barcelona tangu ajiunge nayo akitokea Lyon mwaka 2007.
    Ameisaidia klabu hiyo ya Catalan kutwaa mataji 13 kati ya 16 kwa zaidi ya misimu mitatu iliyopita, yakiwemo mawili ya Ligi ya Mabingwa, Klabu Bingwa ya Dunia na Super Cup za Ulaya, sambamba na mataji matatu mfululzo ya Ligi ya Hispania na Copa del Rey.
    Abidal aliyeumia nyonga akiichezea Ufaransa mechi ya kirafiki wiki mbili zilizopita, alikuwa miongoni mwa wachezaji ambao Barcelona iliwategemea sana katika vita ya kutetea ubingwa wa la Liga, ambao wanazidiwa pointi 10 na vinara Madrid.
    Barcelona imefuzu Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa na itacheza na Athletic Bilbao katika fainali ya Copa del Rey Mei 25.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MASIKINI ABIDAL, INAWEZA KUWA SOKA NDIO BASI TENA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top