// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MAN CITY YAFA KIUME ULAYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MAN CITY YAFA KIUME ULAYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, March 16, 2012

    MAN CITY YAFA KIUME ULAYA


    MANCHESTER, England
    KLABU ya Manchester City ya England imetolewa katika Europa League kwa hasara ya mabao ya ugenini licha ya ushindi wake wa jana usiku wa mabao 3-2 dhidi ya Sporting Lisbon ya Ureno.
    Matias Fernandez alifunga dakika ya 33 kwa mpira wa adhabu na  Ricky van Wolfswinkel akafunga tena dakika ya 40 kuunenepesha ushindi wa Wareno wa 1-0 kwenye mechi ya kwanza.
    Ikihitaji mabao manne ili kusonga mbele, City ilionekana kama kuzinduka kwa mabao ya Sergio Aguero dakika ya 60 na 82, yaliyofuatiwa na bao la Mario Balotelli dakika ya 75 na kufanya sare ya jumla ya mabao 3-3.
    Lakini huo ndio ulikuwa mwisho wa uwezo wao kwenye Uwanja wa Eithad na mwanzo wa safari ya kuiaga michuano ya Ulaya mwaka huu.
    “Ninajivunia kiwango, (lakini) nimestaajabishwa na mechi hizi mbili, kwa sababu nafikiri kwa mechi zote mbili, hatustahili kusonga mbele,” alisema kocha wa City, Roberto Mancini.
    Matokeo hayo yanamaanisha England hawatakuwa na timu hata moja kwenye Robo Fainali ya michuano hiyo, kufuatia Manchester United kutolewa na Athletic Bilbao mapema jana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY YAFA KIUME ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top