Wayne Rooney ataibeba United leo? |
WAPINZANI wa jiji la Manchester, United na City wako kileleni
kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England, lakini wako mguu nje, mgjuu ndani kwenye
Europa League.
United itakuwa ugenini ikijaribu kulipa kisasi cha 3-2 mbele
ya Athletic Bilbao kesho.
Hofu ni kwamba wachezaji makinda wa Bilbao waliifunika ile
mbaya United kwenye mchezo wa kwanza na wengi wanaamini ndoto za Mashetani hao Wekundu
kubeba taji lolote la Uaya zitazimwa kesho.
Angalau City watakuwa kwenye ardhi ya nyumbani ambako haijafungwa
kwenye michuano ya Ulaya kwa miaka minne, lakini watatakiwa kulipa kisasi cha 1-0
kutoka kwa Sporting Lisbon wiki iliyopita.
Bilbao inawania kuwa moja ya timu tatu za Hispania zilizotinga
Robo Fainali, nyingine zikiwa ni Atletico Madrid na Valencia zote zina faida ya
mabao mawili kutoka mechi za kwanza.
Olympiakos, Twente na AZ Alkmaar zote zina nafasi ya kusonga
mbele zikiingia kwenye mechi za marudiano.
Hii ni mara kwanza kwa Manchester United kupoteza mechi
mfululizo katika michuano ya Ulaya ndani ya miaka 16, kufuatia kutolewa Ligi ya
Mabingwa.
“Tumekuwa tuna mwaka mbaya Ulaya,” alisema kocha wa United, Alex
Ferguson said.
Wachezaji wa United, Nani, Anderson anayesumbuliwa na nyama
za paja kama Antonio Valencia na Tom Cleverley anayeumwa kifundo cha mguu wote
wako shakani kucheza mechi hiyo ya Europa League, wakati Wayne Rooney anatarajiwa
kupiga kazi, ingawa mwishoni mwa wiki wanakabiliwa na mchezo wa ligi dhidi ya Wolves.
Mshambuliaji wa Bilbao, Fernando Llorente na kiungo mchezeshaji
Oscar de Marcos wote walikosa mazoezi mapema wiki hii kuelekea kwenye mechi hii
itakayopigwa Uwanja wa San Mames, wenye uwezo wa kumeza mashabiki 40,000.
Bilbao inawania kutinga Robo Fainali ya michuano hiyo kwa
mara ya kwanza tangu msimu wa 1976-77.
Manchester City watakaoshuka dimbani wakiwa na kumbukumbu ya
kipigo kwenye Ligi Kuu Jumapili, kuna tetesi kwamba watamchezesha Carlos Tevez.
Lakini safu ya ulinzi ya City itaendelea kuwakosa majeruhi Vincent
Kompany (calf) na Joleon Lescott (nyonga) na beki wa kulia, Pablo Zabaleta (nyama
za paja).
Aidha, Phillip Cocu ataanza rasmi kazi yake ya ukocha PSV akiiongoza
timu hiyo ya Uholanzi kujaribu kulipa kisasi cha 4-2 kutoka kwa Valencia na kufuta
gundu la kufungwa mechi tatu mfululizo.
0 comments:
Post a Comment