Davide Ballardini |
KUFUKUZWA
kwa Davide Ballardini Cagliari Jumapili kunamfanya awe kocha wa 15 katika ligi
inayoshirikisha timu 20, Serie A kufukuzwa msimu huu.
Italia
kwa haraka inageuka kuwa tanuri la makocha kwa marais wa klabu kuwatupia virago
mara moja, wanapoona timu zao haziendi vizuri.
Rais
wa Cagliari, Massimo Cellino amefukuza kocha wa tatu katika kipindi kisichozidi
miezi saba.
Agosti
katika kujiandaa na msimu mpya, Sardinians walikuwa wanafundishwa na kocha wa
zamani wa Italia, Roberto Donadoni alifukuzwa baada ya mechi ya kirafiki ambayo
Cagliari pamoja na kushinda, lakini akaondolewa na Massimo Ficcadenti akachukua
nafasi.
Alidumu
kwa miezi isiyozidi mitatu kabla ya Ballardini kuchukua nafasi, ambaye
anafukuzwa ndani ya miezi mine na Ficcadenti akipewa nafasi kubwa ya kurudishwa
kazini.
Miaka
michache iliyopita, kocha wa sasa wa Udinese, Francesco Guidolin alidumu kwa
miaka minne Palermo kati ya 2004 na 2007.
Kufukuzwa
kwa Ballardini kunamaanisha Ligi Kuu ya Italia ndio inaongoza kubadilisha
makocha zaidi ya England iliyobadili wanne hadi sasa, Ujerumani (sita) na
Ufaransa (wanne).
La
Liga nayo inatisha kwa kufukuza makocha, ikiwa imefukuza makocha tisa hadi sasa.
Chini
ya Cagliari, ambayo inasaka kocha wan ne msimu huu, kuna Palermo, Cesena na
Novara ambao wako tayari kwa mechi ya tatu wakati klabu nyingine sita zimefukuza
makocha iliyoanza nao msimu huu.
0 comments:
Post a Comment