Caceres kushoto akimdhibiti Neymar |
KIUNGO
mkabaji chaguo la kwanza la Paraguay, Victor Caceres anawaniwa na klabu kubwa
za Ulaya asajiliwe msimu ujao, kwa mujbiu wa mwakilishi wake.
Baada
ya kucheza soka ya nguvu kwenye Kombe la Dunia 2010 na michuano ya Copa America
mwaka jana, Caceres amejipatia umaarufu mkubwa kama miongoni mwa viungo bora wa
ulinzi.
ETSM,
kampuni ya uwakala wa michezo yenye maskani yake London, ambayo ina mkataba na Caceres,
imethibitisha kwamba vigogo wa Ulaya wameonyesha nia kwa mteja wao, zikiwemo
klabu za England ambazo hakuzitaja jina.
“Wote
tunafahamu kwamba Victor Caceres ni mchezaji wa kiwango cha dunia, muhimu zaidi,
tunahitaji kufanya uamuzi ambao utakuwa na manufaa kwa manufaa yake binafsi na
maendeleo yake," alisema Msemaji wa ETSM.
Mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye pia anaweza kucheza kama beki wa kati, amekuwa
na mafanikio, akitwaa ubingwa wa Paraguay
mara tatu na kucheza mechi zaidi ya 160 katika klabu ya nchini mwake, Libertad.
0 comments:
Post a Comment