Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
linaendelea kupokea maombi ya uenyeji wa kituo cha Fainali za Ligi Daraja la
Kwanza iliyopangwa kuanza Machi 31 mwaka huu ikishirikisha timu
tisa.
Mikoa kadhaa imeshawasilisha
maombi ya uenyeji lakini hakuna ambao umekamilisha masharti ya kulipa sh.
milioni 25 TFF ikiwa ni gharama za uendeshaji wa fainali hizo.
Baadhi ya mikoa ambayo
imeshatuma maombi ya kuwa mwenyeji wa fainali hizo ni Mbeya, Morogoro, Mwanza,
Ruvuma na Tabora. Kamati ya Ligi itatangaza kituo cha fainali hizo baada ya
Machi 15 mwaka huu ambayo ni siku ya mwisho kupokea maombi na kutimiza masharti
yaliyowekwa.
Timu zilizofuzu kucheza hatua ya fainali
kutoka kundi A ni Polisi ya Dar es Salaam, Mgambo Shooting ya Tanga na Transit
Camp ya Dar es Salaam. Kundi B ni Mbeya City Council, Mlale JKT ya Ruvuma na
Tanzania Prisons ya Mbeya wakati kundi C ni Polisi ya Tabora, Polisi ya Morogoro
na Rhino Rangers ya Tabora.
0 comments:
Post a Comment