Kipa wa Ferroviario, Mtanzania Muharammi Mohamed 'Shilton' |
VIGOGO wa Kenya, Gor Mahia leo wamefungishwa vurago katika Kombe
la Shirikisho Afrika baada ya kufungwa 1-0 Ferroviario ya Msumbiji,
inayojivunia kipa Mtyanzania, Muharammi Mohamed Shilton kwenye Uwanja wa Nyayo,
Nairobi.
Matokeo yanamaanisha Gor imefungishwa virago kwa jumla ya
mabao 4-1, kufuatia kufungwa 3-0 kwenye mechi ya kwanza mjini Maputo.
Bao hilo pekee lililoiteketeza Gor lilipatikana dakika
ya30, mfungaji Ibraimo Pilate aliyefumua shuti kali la mbali lililomshinda kipa
Jerim Onyango. Afrika Mashariki ni timu mbili tu zimebaki kwenye michuano ya
Afrika, Simba ya Tanzania na URA ya Uganda ambazo ziote zinacheza Ligi ya
Mabingwa.
0 comments:
Post a Comment