// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KEITA, MUNTARI, DIOUF NA WAAFRKA WENGINE WALIONG'ARA ULAYA WIKIENDI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KEITA, MUNTARI, DIOUF NA WAAFRKA WENGINE WALIONG'ARA ULAYA WIKIENDI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, March 05, 2012

    KEITA, MUNTARI, DIOUF NA WAAFRKA WENGINE WALIONG'ARA ULAYA WIKIENDI


    KIUNGO mtaalamu wa Mali, Seydou Keitaalitupia mopira nyavuni zikiwa zimesalia dakika 10 na kuiwezesha Barcelona iliyokuwa pungufu ya mchezaji mmoja kuibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Sporting Gijon katika La Liga mwishoni mwa wiki.
    Bao hilo liliifanya Barca inayoshika nafasi ya pili La Liga iongoze kabla ya kupata linguine baadaye na kuwafanya mabingwa hao wa dunia, Ulaya na Hispania sasa wawe wanazidiwa pointi 10 tu na vinara Real Madrid, zikiwa zimebaki raundi 13 ligi kumaluizika.
    Mshambuliaji wa Misri, Mohamed Zidan alifunga bao lake la tano Bundesliga, lakini halikuweza kuinusuru timu yajke, Mainz, kupigwa 2-1 na vinara, Borussia Dortmund.

    ENGLAND:
    ALEX SONG (Arsenal)
    Kiungo wa Cameroon, alitoa bonge la pasi kwa Robin van Persie wakati The Gunners wakitoka nyuma na kuifunga Liverpool mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Anfield.
    Pasi hiyo muruwa ya Song, alikutana nayo Van Persie dakika ya mwisho na mshambuliajim huyo wa Kiholanzi akashangilia bao lake la 31 msimu huu kwa kwenda kupiga busu kiatu cha Song.

    STEVEN PIENAAR (Everton)
    Kiungo wa Afrika Kusini alitoa pasi bab-kubwa kwa Royston Drenthe wakati Everton ikitoka 1-1 na QPR. Pasi hiyo tamu ya Pienaar, iliunganishwa kimiani na Drenthe dakika ya 31 na winga wa Kiholanzi Dutch akiwa umbali wa mita 25.

    DIDIER DROGBA (Chelsea)
    Mshambuliaji wa Ivory Coast hakuwa na morali kabisa wakati Chelsea inapigwa ‘kidude’ (1-0) na West Bromwich Albion katika mechi ya mwisho kwa Andre Villas-Boas kuwa kocha wa Blues. Drogba alipata nafasi za kufunga na AVB akafukuzwa ndani ya saa 24 baada ya kipigo hicho, ambacho kinawaacha Chelsea nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu.

    CHEICK TIOTE (Newcastle)
    Kiungo wa Ivory Coast, alihusishwa na kadi nyekundu ya utata aliyopewa kiungo wa Benin, Stephane Sessegnon katika sare ya 1-1 dhidi ya Sunderland.
    Sessegnon alimtoa njiani kwa bega Tiote dakika ya 58 ambalo lilikuwa tukio la kawaida la kimchezo, lakini nyota huyo wa Newcastle alijiangusha ‘kiugizaji’ na kumfanya refa atoe kadi nyekundu.

    MAHAMADOU DIARRA (Fulham)
    Kiungo huyo wa Mali, aliichezea mechi ya kwanza Fulham na kutoa pasi ya bao, wakati Cottagers wakiitandika Wolves mabao 5-0. Nyota huyo wa zamani wa Real Madrid, Diarra, aliyejiunga na kikosi cha Martin Jol kama mchezaji huru mwezi uliopita, baada ya kutemwa na Monaco, alitumia muda mwingi kuonyesha uwezo wake baada ya kutokea benchi dakika ya 69 na pasi yake iliunganishwa vema nyavuni na Clint Dempsey.

    UFARANSA:
    SIAKA TIENE (Paris Saint-Germain)
    Tiene aliichezea mechi ya kwanza PSG tangu aiwakilishe Ivory Coast kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Ajaccio, ambao unaifanya timu ya Carlo Ancelotti kurejea kileleni mwa Ligi Kuu.
    Akichukua nafasi ya majeruhi Maxwell zikiwa zimesalia dakika 14, Tiene alisaidai kutengeneza bao la nne la PSG kwa kumimina krosi nzuri iliyounganishwa kimiani na Clement Chantome.

    AYMEN ABDENNOUR (Toulouse)
    Beki wa kati wa Tunisia, Abdennour alifunga bao pekee na kuifanya Toulouse kupata ushindi mzuri wa 1-0 dhidi ya Marseille, ambao unaipandisha timu hiyo hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi. Abdennour alifunga dakika ya 66, baada ya kwenda hewani zaidi ya Souleymane Diawara na kipa wa Marseille, Steve Mandanda kuifuata kona iliyochongwa kutoka wingi ya kulia na Etienne Didot na kuitumbukiza nyavuni kwa kichwa.

    JONATHAN PITROIPA (Rennes)
    Winga wa Burkina Faso, Pitroipa alikuwa nyota wa mchezo wakati Rennes inawafunga wapinzan wao wa Brittany, Lorient mabao 2-0  na kupaa hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligue 1.
    Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25, alimalizia shambulizi zuri la kushitukiza na kuwafungia wageni bao la kuongoza dakika ya 41, kisha akamsetia mchezaji mwenzake wa Morocco, Youssouf Hadji kuifungia Rennes bao la pili zikiwa zimesalia dakika 11.

    UJERUMANI:
    MOHAMED ZIDAN (Mainz 05)
    Mshambuliaji wa Misri sasa amefunga katika mechi tano mfululizo , lakini hakuweza kuiepusha timu yake na kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa klabu yake ya zamani, Borussia Dortmund, ambayo aliachana nayo Januari tu.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30, aliisawazishia Mainz kwa umahiri wa hali ya juu dakika ya 74, lakini Dortmund ikapiga la ushindi dakika tatu baadaye, wakati Mjapan Shinji Kagawa alipotumbukiza nyavuni mpira.

    MAME BIRAM DIOUF (Hanover 96)
    Mshambuliaji wa Senegal, ambaye alijiunga na Hanover Januari akitokea Manchester United, alifunga bao lake la pili katika mechi tano wakati timu yake mpya ikitoka sare ya 2-2 na Augsburg.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alipiga bao hilo kwa kichwa dakika ya 69, kabla Augsburg kusawazisha kupitia kwa Jan-Ingwer Callsen-Bracker kwa penalti dakika ya 89, baada ya kiungo wa Cameroon, Marcel Ndjeng kuchezewa rafu.

    ITALIA:
    SULLEY MUNTARI (AC Milan)
    Nyota wa AC Milan, ambaye alicheza vema mno katika sare ya 1-1 na Juventus wiki iliyopita, alipiga tena kazi nzuri katikam ushindi wa 4-0 dhidi ya Palermo, akimsetia Zlatan Ibrahimovic bao lake la kwanza kati ya mtatu aliyofunga dakika ya 21.

    BOUKARY DRAME (Chievo)
    Beki Msenegali aliyezaliwa Ufaransa, aliipa Chievo sare ya 1-1 na wawania ubingwa, Juventus,akifunga bao dakika ya 76, baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Davide Moscardelli.

    HISPANIA
    SOFIANE FEGHOULI (Valencia)
    Mualgeria alifunga bao la ushindi, Valencia iking’ara ugenini kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Granada, ambao unaiimarisha timu hiyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi.
    Bao hilo lilikamilisha wiki nzuri kwa kiungo huyo, ambaye alifunga bao la ushindi akiichezea kwa mara ya kwanza timu yake ya taifa, dhidi ya Gambia Jumatano.

    FORMOSE MENDY (Sporting Gijon)
    Winga wa Senegal, alicheza dakika zote kwa mara ya kwanza katika klabu yake, Gijon ikipigwa mabao 3-1 na Barcelona kwenye Uwanja wa Camp Nou.
    Mendy, ambaye alianzia kazi Ufaransa, alifanya klazi nzuri kwa kuitengenezea bao la kusawazisha Sporting kipindi cha pili, akitoa krosi kwa Davd Barral aliyefunga.
    SEYDOU KEITA (Barcelona)
    Barcelona ilikuwa kwenye vita ya kung’oa pointi tatu, ikiwa na wachezaji 10 tu uwanjani hadi guu la kushoto la kiungo wa Mali zikiwa zimesalia dakika 10 lilipofanisha vita hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KEITA, MUNTARI, DIOUF NA WAAFRKA WENGINE WALIONG'ARA ULAYA WIKIENDI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top