// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KASHESHE YANGA NA AZAM TAIFA JIONI YA LEO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KASHESHE YANGA NA AZAM TAIFA JIONI YA LEO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 10, 2012

    KASHESHE YANGA NA AZAM TAIFA JIONI YA LEO


    Kikosi cha Yanga, ambacho leo jioni kitakuwa na kasheshe mbele ya Azam

    NYASI za Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zitawaka moto leo kwa mechi kali ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara yenye mvuto wa michuano ya Afrika, kama Kombe la Shirikisho na Ligi ya Mabingwa.
    Yanga inashuka dimbani kumenyana na Azam, ikiwa ina hasira nao ile mbaya Wana Lamba Lamba hao.
    Hasira za Yanga zinatokana na nini? Kwanza wamefungwa na Zamalek na kutolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika mapema kama ilivyo kawaida yao.
    Lakini pili, Yanga imefungwa na Azam mara mbili mfululizo- kwanza kwenye mechi ya Ligi Kuu 1-0 kwenye Ligi Kuu Septemba 18, mwaka jana Uwanja wa Taifa na baadaye kwenye Kombe la Mapinduzi Januari, mwaka huu.
    Lakini yote tisa, 10 ni kwamba Yanga inataka kupoza machungu ya mashabiki wake baada ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa- hivyo Jumamosi watataka kushinda kwa lazima, licha ya ubora wa Azam wanaoutambua.       
    Yanga iliyorejea Jumatatu kutoka Cairo, inasifiwa kucheza soka ya kuvutia licha ya kufungwa na Zamalek, jambo ambalo linawafanya mashabiki wa timu hiyo wawe na hamu kubwa ya kuiona timu yao.
    Mechi ya Jumamosi itawakutanisha vinara wa mabao katika Ligi Kuu, John Bocco kwa upande wa Azam anayeongoza kwa mabao yake 12 na Kenneth Asamoah kwa Yanga, anayefuatia kwa mabao yake 10.
    Lakini pia itawakutanisha makipa wanaowania kumvua glavu Juma Kaseja katika timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mwadini Ally wa Azam na Shaaban Kado wa Yanga ambao wote ni makipa wa akiba katika kikosi cha Mdenmark Jan Borge Poulsen.
    Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima kwa sasa unaweza kusema ndiye mchezaji bora zaidi wa kigeni katika Ligi Kuu- lakini Azam pia ina viungo wazuri wazawa kama Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Abdi Kassim ‘Babbi’ na Jabir Aziz, ambao wote wanaifanya mechi hiyo iwe na ‘quality’ za Afrika.
    Kocha Muingereza Stewart Hall, baada ya kutwaa Kombe la Mapinduzi Januari mwaka huu, katika michuano iliyoshirikisha Simba na Yanga, tena akizifunga timu zote hizo, ameweka bayana sasa anataka kufuta utawala wa vigogo hao na kwenye Ligi Kuu ya Bara.
    Lakini kocha aliyekalia kuti kavu Yanga, Mserbia Kostadin Bozidar Papic hatahitaji presha zaidi na dawa ya kuepuka hali hiyo ni ushindi tu Jumamosi.
    Mambo mengine yanayoifanya mechi hiyo iwe tamu ni kwamba Azam ina wachezaji ambao misimu michache iliyopita walikuwa wanang’ara Yanga, kama Mrisho Ngassa na Abdi Kassim.  
    Kocha wa Azam, Muingereza Steward Hall anaingia kwenye mchezo akiwa kumbukumbu ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Coastal Union, wakati Mserbia wa Yanga, Kostadin Papic ana hasira za kipigo cha Cairo.

    REKODI YA YANGA AZAM FC:
    Septemba 18, 2011
    Azam 1-0 Yanga
    Machi 30, 2011
    Yanga 2-1 Azam
    Oktoba 24, 2010
    Azam 0-0 Yanga
    Machi 7, 2010
    Yanga 2-1 Azam           
    Oktoba 17, 2009
    Azam 1-1 Yanga     
    Aprili 8, 2009
    Yanga 2-3 Azam FC 
    Oktoba 15, 2008
    Azam FC 1-3 Yanga

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KASHESHE YANGA NA AZAM TAIFA JIONI YA LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top