Kapteni Steve |
NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard amewataka wachezaji wenzake
wa timu hiyo ya Anfield kujituma haswa baada ya kupokea kipigo cha tatu
mfululizo kutoka kwa Sunderland Jumamosi.
Wekundu hao hawajawahi kufungwa mechi tatu mfululizo tangu mwaka
2003, na kipigo hicho kinamuacha kocha Kenny Dalglish katika nafasi ya saba
kwenye msimamo wa ligi, pointi mbili tu dhidi ya wapinzani wao Everton watakaomenyana
nao katika Merseyside derby Uwanja wa Anfield.
"Wachezaji wanatakiwa kuwajibika kwa hapa tulipo kwenye
ligi," alisema Gerrard said. Si nzuri kiasi cha kutosha kwa klabu kama
yetu kuwa huko. Tunatakiwa kutafuta kiwango kizuri na cha kudumu. Tunahitaji kufanya
kweli na hakuna timu nzuri ya kuifanyia hivyo zaidi ya Everton.
Baada ya kutwaa Kombe la Ligi mwezi uliopita na kumaliza ukame
wa mataji wa miaka sita, Liverpool imefufua matumaini ya kupigania Nne Bora
katika Ligi ili icheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao.
0 comments:
Post a Comment