KLABU ya Juventus ilipoteza nafasi ya kulingana kwa pointi
na AC Milan Jumatano baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Bologna.
Nahodha wa Bologna, mwenye umri wa miaka 35, Marco Di Vaio aliwafungia
bao la kuongoza wenyeji dakika ya 17 na Mirko Vucinic akaisawazisha Juve dakika
ya 58.
Mechi hiyo iliahirishwa kutoka wiki iliyopita kutokana na
hali ya barafu na sasa Milan inaiacha Juve kwa pointi mbili, timu zote zikiwa
zimecheza mechi sawa.
Habari mbaya kwa Juve ni kwamba, beki wake Leonardo Bonucci alilimwa
kadi ya pili ya njano dakika ya 84 na kukiacha Kibibi Kizee cha Turin kiende
Genoa bila mabeki wake watatu Jumapili kuwavaa wenyeji wao hao.
Kocha anayeinoa Juventus katika mwaka wake wa kwanza, Antonio
Conte pia alilimwa kadi nyekundu kiama kinga dakika ya 72.
Juventus inabakia kuwa pekee ambayo haijafungwa katika ligi
ya Itali, lakini ndio pia iliyotoa droo nyingi—13— na imeshinda mechi moja tu
katika ya sita zilizopita. Juve pia ilitoka 1-1 na Chievo Verona wi9ki
iliyopita.
0 comments:
Post a Comment