Rooney wa Man Utd |
Van Persie wa Arsenal |
Gerard wa Liverpool anarudi kazini |
Dzeko wa Man City |
BAADA ya kupunguza deni la pointi katika mbio za farasi
wawili za kuwania taji la Ligi kuu England, Manchester United inatarajiwa
kuendeleza mbio zake za kuifukuza Manchester City katika miezi miwili ya mwisho
ya msimu.
United imepitia katika njia ngumu na kutoka salama ikishinda
dhidi ya Arsenal, Liverpool na Tottenham—wakati pia ilitoka nyuma kwa mabao 3-0
na kupata sare ya 3-3 na Chelsea — hivyo kubaki inazidiwa pointi mbili na City zikiwa
zimebaki mechi 11 ligi kuisha.
Ikiwa inakabiliwa na mechi ya wapinzani wa jadi dhidi ya City
Aprili 30, mechi zilizobaki za United ni rahisi mno kulinganisha na za
wapinzani wao.
Wanaanza na West Bromwich Albion, ambayo imeshinda mechi zake
tatu zilizopita, lakini ni kibonde mno anayekwenda Old Trafford.
Zikitoka kutolewa nishai katika mechi ya kwanza ya Europa
League hatua ya 16 bora Alhamisi, Manchester zote lazima ziwahahakishie
mashabiki wake kwamba hazina ‘hangover’ wakati zinaporejea kwenye Ligi Kuu mwishoni
mwa wiki.
Wakati United iliyolipigwa 3-2 nyumbani na Athletic Bilbao
wanaikaribisha WBA leo, City waliopigwa 1-0 na Sporting Lisbon ugenini
wataifuata Swansea, ambayo imefungwa mechi mbili tu kati ya mechi zake 13 za
nyumbani msimu huu tangu ipande.
City imeshinda mechi zake zake nne zilizopita za ligi,
lakini itamkosa beki wake wa nguvu, Vincent Kompany aliyeumia Ureno.
United iliifunga Tottenham 3-1 wiki iliyopita na kuwaacha
kwa pointi 11 Suprs wanaofundishwa na Harry Redknapp katika nafasi ya tatu.
Baada ya kupigwa mechi mbili mfululizo na Arsenal na United,
Spurs leo wanatarahjiwa kujipoza machungu kwa Everton, wakiwa wanaizidi kwa
pointi nne Arsenal inayoshika nafasi ya nne.
Arsenal iliyotolewa ‘kiume’ katika Ligi ya Mabingwa,
itaikaribisha Newcastle Jumatatu, wakati Chelsea inayoshika nafasi ya tano itakuwa
mwenyeji wa Stoke hiyo ikiwa mechi ya kwanza ya ligi ya Roberto Di Matteo tangu
arithi mikoba ya boasi wake, Villas-Boas.
Liverpool wanaweza kuwa nao tena Steven Gerrard na Glen
Johnson waliokuwa majeruhi katika mchezo wa leo na Sunderland.
Wigan itaifuata Norwich kesho, wakati Bolton itakuwa
mwenyeji wa Queens Park Rangers na Wolverhampton Wanderers watakuwa nyumbani
wakiikaribisha Blackburn leo. Fulham watasafiri kuwafuata Aston Villa.
0 comments:
Post a Comment