// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); HARUNA HAKIZIMANA FADHIL NIYONZIMA: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE HARUNA HAKIZIMANA FADHIL NIYONZIMA: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, March 14, 2012

    HARUNA HAKIZIMANA FADHIL NIYONZIMA:


    Niyonzima kulia akimiliki mpira mbele ya Nassor Masoud 'Chollo' wa Simba 
    KATI ya wachezaji wapya wa kigeni walioingia kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima ndiye ambaye alikuwa gumzo zaidi, kwa sababu wengi hawakuamini kama klabu yake, APR ya Rwanda ingeweza kumuachia.
    Lakini historia imetimia, Niyonzima maarufu kama Fabregas kwa mashabiki wa Tanzania amejiunga na Yanga ya Dar es Salaam na sasa anaonyesha cheche zake katika ligi hiyo.
    Baada ya kucheza mechi kadhaa za ligi ya Tanzania, Niyonzima anasema kwamba amegundua kwa sasa ligi ya nchi hii imeipiku ligi ya Rwanda.
    “Ligi yetu (Rwanda) ilikuwa juu sana, lakini mwaka jana imeshuka mno. Baada ya kucheza hizi mechi mbili, nimegundua ligi ya Tanzania ni ngumu na ina msisimko mkubwa.
    Niyonzima anasema msisimko wa kishabiki, morali ya wachezaji na maandalizi ya ligi yenyewe ni miongoni mwa vitu vinavyoifanya ligi ya Tanzania iwe bora kwa sasa, hata yeye anaicheza huku akiifurahia.
    “Yaani sasa hivi hakuna mechi ndogo kwenye ligi ya Tanzania, kila mechi ni ngumu. Ni ligi yenye ushindani haswa, ninafurahia kucheza,” anasema. 
    Kabla ya kuja Yanga, Niyonzima amewahi kufanya majaribio mara mbili Ufaransa, mara moja Sweden na mara moja Ujerumani na kote alifuzu, lakini hadi leo bado analikoga vumbi la Afrika, kwa nini?
    “Majaribio ya Sweden, Ujerumani na Ufaransa kote APR walinifanyia roho mbaya, waliziwekea vikwazo zile timu zikaamua kuachana na mimi. Nikapata timu ya kuninunua ya Morocco, lakini APR ikaniwekea ngumu pia,” anasema.
    Kutokana na kuzibiwa riziki zake za kucheza Ulaya na timu hiyo ya jeshi la Rwanda, Niyonzima anasema aliweka nadhiri akimaliza mkataba wake asiongeze tena.
    “Nikiwa bado APR wakati nimekwishazungumza na Yanga, nikapata nafasi ya kwenda  Ubelgiji kwa majaribio, lakini nikashindwa kwenda kwa sababu nilijua hata nikienda APR hawataniruhusu, nikaona nimalizane nao kwanza, nije Yanga.
    “Yanga katika mkataba wao na mimi tumekubaliana nikipata timu tu nje, wananiruhusu niondoke, hakuna tatizo. Na ninapenda niwaambie mashabiki wa Yanga najisikia furaha sana kuchezea timu hii,” anasema Niyonzima, mume wa Wimezanaila, aliyezaa naye watoto wawili wa kiume, Niyonzima na wa kike Halila.
    Je, Niyonzima angependa mwanae wa kiume arithi mikoba yake kwenye soka? “Hapana, sitaki kabisa acheze mpira,” anasema.
    Kwa nini? “Sitaki tu acheze, mimi ninataka asome sana, ila ikitokea yeye mwenyewe akaamua kucheza, sitamzuia, sitaki kwa sababu soka yetu hii tunacheza ina machungu mengi sana ambayo sitaki mwanangu ayapate,” anasema.
    Mchezaji gani Tanzania anamvutia Niyonzima? “Mrisho Ngassa, nasikitika nimekuja Yanga sikumkuta. Wakati nikiwa APR niliushawishi uongozi umsajili, ukashindwa, na mimi ilikuwa nije Yanga tangu mwaka juzi kwa sababu yake, ila APR wakanibania,” anasema.
    Ulaya je, Niyonzima anavutiwa na mchezaji gani? “Yes, Andres Iniesta,” anasema akimaanisha anavutiwa na nyota huyo wa Hispania na Barcelona.
    Anazungumziaje mechi ijayo ya watani wa jadi katika soka ya Tanzania, ambayo kwake itakuwa ya pili kucheza baada ya ile ya Ngao ya Jamii, Agosti 17, ambayo Yanga ilifungwa mabao 2-0.
    “Tuko vizuri kwa sasa na tumejiandaa vema, tuna matumaini ya kushinda Jumamosi. Simba ni timu nzuri, lakini na sisi tuko vizuri kwa sasa na watu watajionea Jumamosi,”alisema.
    Aidha, Fabregas huyo wa Yanga ameweka nadhiri ya kupigana kufa na kupona kuhakikisha anatikisa nyavu za Simba Jumamosi.
    “Nataka niwape raha Yanga, nataka niwafunge Simba. Nitaingia uwanjani kwa nia ya kuwafunga,”anasema.
    Naam, huyo ndiye kiungo mpya wa Yanga, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima, aliyepania kuwatungua Simba kwenye ligi, ili kulipa kisasi cha kipigo cha Ngao ya Jamii.
    Je, ataweza kutimiza nadhiri yake hiyo? Bila shaka hilo ni jambo la kusubiri na kuona.

    WASIFU WAKE:
    JINA: Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima
    KUZALIWA: Aprili 7, 1991
    ALIPOZALIWA: Kigali, Rwanda
    KLABU YAKE: Yanga SC
    KLABU ZA AWALI:
    Mwaka            Klabu
    2009-2011       APR FC
    2006-2008       Rayon Sport 
    (Tangu 2006, ameichezea Rwanda mechi 35 ameifungia mabao 12)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HARUNA HAKIZIMANA FADHIL NIYONZIMA: Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top