Ray Barlow |
KLABU ya West Bromwich Albion leo imetoa salamu za rambirambi
kwa gwiji wake, Ray Barlow kufuatia kifo chake jana akiwa katika umri wa miaka 85.
Barlow, alijiunga na The Baggies akiwa na umri wa miaka 18 mwaka
1944 na kuichezea timu hiyo mechi 482 na pia aliichezea mechi moja timu ya
taifa ya England.
Mara ya mwisho alikuwamo kwenye kikosi cha The Baggies kilichotwaa
Kombe la FA mwaka 1954 wakiifunga Preston mabao 3-2 na mwaka 2004 alitajwa kama
mmoja wa wachezaji 16 magwiji wa West Brom katika uchaguzi uliokwenda sambamba
na sherehe za miaka 125 ya klabu hiyo.
0 comments:
Post a Comment