Steven Gerrard (kushoto) akishangilia bao lake la pili.
|
KIUNGO Steven Gerrard jana amecheza mechi yake ya 400 ya
Ligi Kuu ya England na kupiga mabao matatu peke yake akiiongoza Liverpool kushinda
3-0 dhidi ya wapinzani wao wa jadi, Everton.
Gerrard alifunga bao la kwanza dakika ya 34 baada ya kufumua
shuti lililowapita mabeki watatu na kipa Tim Howard. Kiungo huyo mkongwe wa England,
baadaye alifunga mabao mawili kwa jitihada za Luis Suarez dakika ya 51 na
dakika za majeruhi.
Pamoja na ushindi huo, kuwa ndani ya Top-Four bado
inaonekana kuwa maji marefu kwa Liverpool, ingawa sasa Wekundu hao wanaizidi
pointi tano Everton wakielekea kwenye fainali ya Kombe la FA Jumapili dhidi ya Stoke.
Tayari Liverpool imetwaa Kombe la Ligi na kujihakikishia
kucheza michuano ya Ulaya msimu ujao. Sasa inapigania kumaliza juu ya Everton kwa
msimu wa saba mfululizo.
0 comments:
Post a Comment