KOCHA wa Manchester
United, Sir Alex Ferguson amesema mechi dhidi yao na
Tottenham leo ndiyo ngumu katika jitihada za
kutetea taji la klabu yake na kuingoa Man.city kutoka kileleni.
Tottenham ikiwa katika nafasi ya tatu nyuma ya Manchester United ndiyo bado imechapwa na Arsenal 5-2 ikimkosa kiungo wake Scott Parker anayetumikia kifungo cha kadi nyekundu.
Kutokuepo kwa kiungo Parker ni pigo kubwa kwa Spurs, amesema meneja wa klabu hio Harry Redknap.
Hata hivyo mtaalamu huyo wa soka anasema ataziba mapengo hayo kwa kutumia wachezaji kama Sandro na Jake Livermore ikiwa fursa kwao kuonyesha uwezo wao.
Tabia ya kuziba mapengo si tatizo kwa United ambayo inakumbuka Willem Korsten aliyefunga mawili kwenye uwanja wa White Hart Lane kuipa Spurs 3-1 dhidi ya Timu ambayo tayari ilikua imeisha tangazwa mshindi wa Ligi ya mwaka 2000-01
Ryan Giggs na Paul Scholes wote walishiriki pambano hilo na huenda wakawepo jumapili wakati Giggs akisherehekea mechi yake ya 900 akichezea.
0 comments:
Post a Comment