// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); FELIX MUMBA SUNZU JR: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE FELIX MUMBA SUNZU JR: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, March 14, 2012

    FELIX MUMBA SUNZU JR:


    KATIKA mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii kati ya Simba na Yanga, uliofanyika katikati ya wiki ulileta furaha na huzuni kwa upande mmoja. Kuna waliofurahia na wale waliolala mapema sikuhiyo.
    Mchezo huo ambao unaashiria kuanza kwa Ligi Kuu, ulizikutanisha timu hizo ambapo Simba ilifanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 2-0.
    Katika mabao hayo, moja lilifungwa na Haruna Moshi ‘Boban’ huku jingine likiwekwa kimiani na Felix Sunzu Jr, ambaye pia ndiye aliyetengeneza bao lililopachikwa na Boban.
    Kwa sasa amekuwa jina kubwa na limekaa mno midomoni mwa washabiki wa Simba, ambao wanaona ni suluhisho la timu hiyo katika safu ya ushambuliaji.
    Kumbuka mchezaji huyu wa zamani wa Konkola Blades ya Zambia na anayeichezea pia timu ya taifa ya nchi hiyo, Chipolopolo, aliachwa na Al Hilal inyonolewa na Srojdevic Milutin ‘Micho’ ikiwa ni miezi sita tu toka atwaliwe na timu hiyo.
    Al Hilal waliamua kuvunja mkataba na Sunzu, baada ya mshambuliaji huyo kudaiwa kuonyesha kiwango kibovu na kuzidiwa ujanja na Mzimbabwe Sadomba, aliyeonekana kufumania mno nyavu.
    “Ni kweli, Al Hilal imeamua kusitisha mkataba wake na Sunzu, baada ya kuvunjwa moyo na kiwango duni alichoonyesha na kocha ameamua kutomchukua kabisa,” ilisema taarifa ya klabu hiyo.
    Sunzu Jr alionwa na Micho, baada ya kuonyesha kiwango kikubwa katika michuano ya Kombe la Chalenji mwaka jana, ambapo alikuwa akiichezea Zambia.
    Kwa muda Sunzu, anaonekana kama anayehangaika barabarani na kushindwa kutulia katika timu moja kwani baada ya kuwemo katika kikosi cha Zambia 2008, alichukuliwa na Al Masry ya Tunisia, ambako nako alitemwa kwa sababu kama hizo.
    Aliporudi Zambia, aliamua kujiunga na timu ya nyumbani kwao ya Konkola Blades, lakini akaondoka na kwenda kujiunga na Lupopo ya Lubumbashi, mwaka 2010 na yaliposhindikana alirejea tena Konkola Blades kwa mara ya tatu.
    Katika michuano ya Kombe la Chalenji, Sunzu akaonyesha kiwango kikubwa na kufanikiwa kufunga mabao matano, hivyo kuivutia Al Hilal iliyoamua kumchukua.
    Sunzu akajumuishwa katika ziara ya timu hiyo huko Misri na Israel kabla ya kuchukuliwa na Al Hilal, huku kukiwa na madai TP Mazembe nayo inamtaka, timu ambayo anachezea pia ndugu yake, Stopilla.
    Baada ya Al Hilal kumtema, Simba ikaingia kati na kuanzia kumfuatilia mshambuliaji huyo na awali timu hiyo ilionekana kutaka kuiingiza Simba ‘king’ kwa madai bado haijamtema ili ipate fedha.
    Sunzu, anaonekana ni mkali akiwa zaidi na Wazambia wenzake kwani alikuwa ndiye mfungaji bora wa michuano ya Chalenji 2010.
    Wakati huo Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geodfrey Nyange ‘Kaburu’ alisema wako katika mazungumzo ya kina ya kuhakikisha wanamtwaa mshambuliaji huyo.
    “Ni mmoja kati ya wachezaji wazuri zaidi na naamini akifika hapa atatusaidia kwa kiwango kikubwa, kwani ana uwezo mkubwa ambao utaisaidia zaidi Simba,” alisema Kaburu wakati huo.
    Kwa sasa imeonekana kweli, kwani Sunzu ameondokea kuwa mshambuliaji tumaini ndani ya Simba na anayeweza kuisaidia zaidi katika Ligi Kuu iliyoanza jana.
    Ni nani?
    Felix Mumba Sunzu alizaliwa Mei 2, 1989 katika mji wa Chingola nchini Zambia, ambaye kwa sasa anaichezea Simba.

    Sunzu alianza maisha ya soka kwa kuichezea Afrisport F.C na mwaka 2005 alijiunga na timu aliyoichezea baba yake ya Konkola Blades, lakini baada ya mwaka mmoja wa kuichezea timu ya vijana mwaka 2007 akapandishwa hadi timu ya wakubwa.
    Katika msimu wake wa kwanza aliichezea Konkola Blades mechi 25 na kufunga mabao 15, lakini Februari 2007 akachukuliwa kwa mkopo na timu ya AS Marsa, ambapo alicheza mechi 16 na kufunga mabao mawili katika Ligi Kuu ya Tunisia.
    Lakini Juni 2008 akarudi Konkola Blades lakini Septemba 2, 2008 akapelekwa kwa mkopo katika timu ya LB Chateauroux inayoshiriki Ligi Daraja la Pili Ufaransa kwa muda wa mwaka mmoja.
    Julai 2009 akarudi AS Marsa ambaye alicheza Oktoba 29, kabla ya timu hiyo kuamua kuachana naye, ambapo akiwa hapo alicheza mechi mbili tu.
    Alishawahi kukaririwa akisema, kwa sasa amekuja nchini kuhakikisha anarejesha heshima yake na kuwataka mashabiki wa Simba, wasubiri vitu vingi zaidi kutoka kwake.
    Tutake tusitake, Sunzu anaonekana kurudi katika makali, kwani katika mchezo dhidi ya Yanga, alitumia uzoefu wake kuifanya beki ya timu hiyo ionekane imepwaya.
    Ingawa ni mchezo mmoja tu, Sunzu anatakiwa kuonyesha vitu zaidi ili mashabiki wa Simba waendelee kumuamini, kwani kinyume chake anaweza kujikuta akizidi kutangatanga.
    WASIFU
    JINA: Felix Mumba Sunzu
    KUZALIWA: Mei 2, 1989
    ALIPOZALIWA: Chingola, Zambia
    UREFU: Futi 5 inchi 8
    NAFASI: Mshambuliaji
    TIMU: Simba
    JEZI Na: 10
    Timu za Vijana
    2002-2005    Afrisport F.C
    2005-2007    Konkola Blades
    Timu za Wakubwa
    2007- Konkola Blades
    2007-2008    AS Marsa (mkopo)
    2008-2009  LB Châteauroux (mkopo)
    2009   AS Marsa (mkopo)
    Timu ya Taifa
    2005-2007    Zambia U-21
    2008- Zambia

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FELIX MUMBA SUNZU JR: Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top