// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); ENGLAND, UJERUMANI ZAKALIA KUTI KAVU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE ENGLAND, UJERUMANI ZAKALIA KUTI KAVU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, March 13, 2012

    ENGLAND, UJERUMANI ZAKALIA KUTI KAVU


    Cristiano Ronaldo

    ENGLAND na Ujerumani zinaweza zisiwe na timu kwenye robo fainali ya Ligi ya Mabingwa kama Chelsea na Bayern Munich hazitoweza kubadilisha matokeo ya kufungwa kwenye michezo ya kwanza.
    Tofauti na Italia ligi ya Serie A, inayoshutumiwa kwa vurugu za uwanjani, kupungua kwa mashabiki na kushuka kwa thamani ya ligi hiyi, wanaweza kumaliza leo kwa timu zao tatu kufuzu kwa nane bora.
    Chelsea ilifungwa 3-1 kwenye mchezo wa kwanza hivyo wataingia leo kuwakabili Napoli ambao imeshinda mechi zake tano zilizopita za ligi na Ijumaa iliyopita ilichakaza Cagliari kwa mabao 6-3.
    Bayern waliolala kwa bao 1-0 kutokak wa FC Basel, timu isiyotarajiwa pamoja na APOEL Nicosia, watalazimika kumaliza rekodi ya kutokufungwa wa timu hiyo ya Uswisi kama wanataka kusonga mbele.
    Kushindwa kufanya hivyo itakuwa mwisho wa ndoto wa timu hiyo ya Bavaria kucheza fainali itakayofanyika kwenye uwanja wao wa Allianz Arena.
    Michezo mingine leo, ni ule wa Claudio Ranieri atakuwa akiwaongoza Inter Milan, mabingwa wa 2010 kufuta bao1-0 walilofungwa na Olympique Marseille ili kusonga mbele, huku Real Madrid wakitakiwa kumaliza kazi yao kwa CSKA Moscow baada ya kutoka sare 1-1 kwenye baridi kali ya Russia.
    Washindi wa mechi hizo wataungana na mabingwa watetezi Barcelona, mabingwa mara saba AC Milan, Benfica mabingwa mara mbili na timu ndogo ya APOEL kwenye upangwaji wa ratiba ya robo fainali hapo Ijumaa.
    Kuondolewa kwa Chelsea kuitaifanya Ligi Kuu ya England kwa mara ya kwanza kukosa timu kwenye robo fainali tangu msimu wa  1995/96.
    Arsenal ilitolewa wiki iliyopita, pamoja na kushinda3-0 dhidi ya Milan haukutosha kuwavusha baada kufungwa 4-0 kwenye mchezo wa kwanza, huku Manchester United na Manchester City zikishindwa kufuzu hatua ya makundi.
    Mabingwa wa Ujerumani, Borussia Dortmund walitolewa hatua ya makundi huku Bayer Leverkusen wakizamishwa na Barcelona, kwa kufungwa 7-1 kwenye Uwanja wa Nou Camp wiki iliyopita kwa ujumla wa mabao 10-2.
    Hivyo kuicha Bayern Munich pekee kupeperusha bendera ya Bundesliga, ambayo msimu ujao watapata nafasi ya kuingiza timu tatu moja kwa moja kwa hatua ya makundi kutokana na udhaifu wa  Serie A.
    Napoli, ikiwa kwenye msimu wake mzuri na kukumbusha enzi za Diego Maradona walipotamba kwenye michuano ya Kombe la Ulaya, lakini baada ya hapo hajawahi kwenda mbele zaidi ya hatua ya pili.
    ìEnzi za Maradona zimebaki kuwa za mafanikio zaidi katika historia ya Napoli, lakini tunajihisi kuwa tunakaribia mafanikio hayo ni jambo linalofanya tujisikie faraja,îalisema kocha wa Napoli, Walter Mazzarri.
    Safu yake ya washambuliaji watatu Edinson Cavani, ambaye amefunga mabao matano, Ezequiel Lavezzi na Marek Hamsik wametegeneza moja ya safu hatari zaidi kwa sasa.
    Chelsea wamebadilisha kocha tangu walipocheza mchezo wa kwanza kwa kumteua Roberto Di Matteo kuchukua nafasi ya Andre Villas-Boas aliyetimuliwa.
    Basel itakuwa ikijaribu kuwa timu ya kwanza ya Uswisi kufuzu kwa hatua ya nane bora tangu Grasshoppers ilipofanya hivyo msimu wa 1978/79 wakati huo wa Kombe la Ulaya.
    Bayern imeshinda mechi 11 kati ya 12 za Ulaya ilizocheza nyumbani, japokuwa waliondolewa kwenye hatua hiyo baada ya kufungwa  3-2 na Inter Milan kwenye Uwanja wao wa Allianz Arena.
    Ranieri alinusurika kidogo kukumbwa na janga la Villas-Boas tangu alipofungwa 1-0 na Olympique na kushinda mchezo huo kumebaki taji pekee kwa Inter ambayo kwa sasa imeporomoka hadi nafasi ya saba katika Serie A.
    Kikosi cha Inter katika mchezo wa kwanza kilikuwa na wachezaji wenye wastani wa miaka 31 na siku 331, wakivunja rekodi yao wenyewe ya Ligi ya Mabingwa walipocheza na wachezaji wa umri wa miaka 31 na siku 317 mapema msimu huu walipoikabili Lille.
    Real wakiwa kwenye kiwango cha juu wataikaribisha CSKA jijini Madrid, kwenye mazingira yao ya kujidai tofauti na ile hali hewa ya baridi ya Moscow.
    Timu ya Jose Mourinho ilimaliza hatua ya makundi kwa asilimia 100, japokuwa wanatakiwa kuwa makini na mshambuliaji wa CSKA nyota wa Ivory Coast, Seydou Doumbia ambaye amefunga mabao matano katika mechi sita za Ligi ya Mabingwa msimu huu na rekodi ya kufunga mabao 12 kati ya mechi 13 alizocheza za ligi hiyo kwa miaka miwili iliyopita.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ENGLAND, UJERUMANI ZAKALIA KUTI KAVU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top