// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); EMMANUEL ARNOLD OKWI: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE EMMANUEL ARNOLD OKWI: - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 17, 2012

    EMMANUEL ARNOLD OKWI:


    MSHAMBULIAJI wa Simba Emmanuel Arnold Okwi, pamoja na uhodari mkubwa alionao amejikuta akiingia kwenye matatizo mara kwa mara katika klabu hiyo.
    Okwi aliisaidia timu yake ya taifa ya Uganda The Cranes kutwaa ubingwa wa Kombe CEFACA Tusker Challenge, na alikuwa ni mmoja wa wafungaji bora.
    Pia katika timu yake ya Simba mchezaji huyo amekuwa ni tishio mbali ya kosa kosa nyingi ambazo zimekuwa zikiwakera mashabiki wa timu hiyo ambao huwa wanaona kama anafanya makusudi.
    Mashabiki wengi wa Simba wamekuwa wakikosa imani na mchezaji huyo, hasa pale timu yake inapocheza na Yanga, ambapo huwa anadaiwa kucheza chini ya kiwango.
    Wakati timu yake ikiwa katika maandalizi ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho (CAF) na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Okwi ameshindwa kuripoti katika timu yake tangu aondoke Desemba mwaka jana,  kwa madai kwamba anakwenda kula sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya, lakini hadi leo hajawasili nchini.
    Pamoja na ukimya huo, uongozi wake ulijaribu kumtafuta kwa kumpigia simu yake ya mkononi lakini ilikuwa imezimwa, huku zikizagaa taarifa kwamba mchezaji huyo amekwenda kufanya majaribio Iceland.
    Tangu taarifa hizo ziripotiwe, siku nne kabla uongozi wa Simba ulifanikiwa kumpata baada ya simu yake ya mkononi kuwa hewani, na katika kujitetea kwake Okwi alidai kwamba alikuwa anaumwa.
    Tangu atoe taarifa hizo inakwenda wiki ya pili sasa Okwi hapatikani tena kwenye simu yake ya mkononi, hali ambayo imewafanya viongozi wake waingiwe na hofu.
    Vituko hivyo vya Okwi vinazidi kuwapandisha hasira wana-Simba ambao huwa wanaamini kwamba mchezaji huyo huwa anatumiwa na watani zao Yanga.
    Tukio ambalo litakuja kukumbukwa ni lile la Oktoba 29 mwaka jana, katika mchezo wa Ligi Kuu, baada ya mchezaji huyo kukosa kosa mabao mengi mara baada ya mchezo kumalizika akajikuta akiingia mikononi mwa mchezaji mwenzake, kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ ambaye alikasirishwa na hivyo kumrushia makonde.
    Pamoja na tukio hilo kuonekana wazi, lakini OKwi mwenyewe alikanusha katika vyombo vya habari, huku akitishia kuvishtaki.
    Usumbufu wa Okwi sio Tanzania tu, kwani kuna wakati mchezaji huyo alikwenda Afrika Kusini kufanya majaribio katika klabu ya Kaizer Chief, baada ya kufuzu alitakuwa kupimwa afya yake.
    Lakini siku ambayo alitakiwa kupimwa mchezaji huyo hakutokea, na hivyo madaktari kumsubiri kwa zaidi ya masaa matatu bila mafaniko, hali ambayo ilimfanya wakala wake ajisikie vibaya kwani alioneana kama na yeye ni taapeli.
    Hata alipopatikana mchezaji huyo alidai kwamba alikuwa amefiwa, hivyo siku ambayo alitakiwa kurudi Afrika Kusini alikosa ndege, na hivyo akajikuta anakosa ofa hiyo.
    Itashangaza kama viongozi wa Simba wataendelea kumfumbia macho mchezaji huyo ambaye anaonekana ni mtovu wa nidhamu, atazidi kusumbua na hata wachezaji wenzake watajisikia vibaya kwani wengi wao wanaamini kwamba baadhi ya viongozi wanamlea sana mchezaji huyo.
    Hata hivyo Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema wamemshitaki mchezaji huyo katika Kamati ya Nidhamu ya klabu hiyo, hivyo akitua nchini atatakiwa ajisalimishe katika kamati hiyo na kutoa maelezo kabla hatua nyingine hazijafuatwa.
    Okwi  alijiunga na Simba mwaka 2010 akitokea katika klabu ya SC Villa ya Uganda na pia ni mchezaji wa timu yake ya taifa ya Uganda The Cranes.
    Pia mchezaji huyo aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa, mkataba wake ukimalizika ndani ya timu hiyo, kama Yanga watamuhitaji yupo tayari kuichezea, wakati huo Yanga ilikuwa ikinolewa na Mganda mwenzake, Sam Timbe ambaye alifungashiwa virago na waajiri wake, na hivyo mikoba yake kurithi Mserbia Kostadin Papic.

    WASIFU WAKE:
    JINA: Emmanuel Arnold Okwi 
    KUZALIWA: Desemba 25, 1992
    ALIPOZALIWA: Kampala, Uganda 
    KLABU YAKE: Simba SC
    KUJIUNGA: 2008
    NAFASI: Mshambuliaji
    KLABU ZA AWALI:
    2006-2008: SC Villa (Uganda)

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: EMMANUEL ARNOLD OKWI: Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top